Akilitz Technologies

Ni wataalama walio bobea katika Teknologia ya habari na mawasiliano ya Kompyuta na mitandao ya inteneti

This is default featured post 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Jumatatu, 15 Julai 2013

CCM Chali, Chadema yaibuka kidedea Arusha

Chadema kimethibitisha umwamba wake katika siasa za Jimbo la Arusha Mjini, baada ya kutetea kwa kishindo kata zake nne kwenye uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika jana.
Katika uchaguzi huo uliokuwa unasubiriwa kwa hamu na ambao ulichukuliwa kama kipimo cha siasa za Arusha ambazo zimekuwa na mvutano mkubwa, Chadema kiliongoza katikia vituo vyote 136 vya kupigia kura Kata za Elerai, Kaloleni, Kimandolu na Themi.
Kata hizo zilikuwa wazi tangu mwaka 2011 baada ya Chadema kuwatimua wanachama wake waliokuwa madiwani Estomih Mallah(Kimandolu), John Bayo (Elerai), Reuben Ngowi (Themi) na Charles Mpanda (Kaloleni).
Matokeo
Katika matokeo yaliyotangazwa na Msimamizi wa Uchaguzi Kata ya Elerai, Obedi Meng’oriki mshindi alikuwa Jeremiah Mpinga wa Chadema aliyepata kura 2,047 dhidi ya 1,471 za Emmanuel Laizer wa CCM. Katika Kata hiyo kulikuwa na wagombea wengine ambao ni John Bayo (CUF; kura 302), Seif Shimba (CCK; kura 3) na Boisafi Shirima (TLP;1).
Katika Kata ya Themi, Kinabo Edmund wa Chadema aliibuka na ushindi baada ya kupata kura kupata kura 674. Msimamizi wa Uchaguzi Kata hiyo, Ezeka Mboya alisema Kinabo alifuatiwa na Victor Mkolwe aliyepata kura 326 na Lobora Ndarpoi wa CUF alipata kura 307.
Kata ya Kaloleni, Msimamizi wa Uchaguzi, Anna Ledisa alimtangaza Kessi Lewi wa Chadema kuwa mshindi kwa kura 1,470 dhidi ya Emmanuel Mliari wa CCM aliyepata kura 330 na Abbas Mkindi wa CUF aliyepata kura 275 na Ngilishi Pauli wa Demokrasia Makini aliyeambulia kura mbili.
Kata ya Kimandolu, Msimamizi wa Uchaguzi, Suleiman Kilingo alimtangaza Mchungaji Rayson Ngowi wa Chadema kuwa mshindi kwa kura 2,761 na kumshinda Edna Saul wa CCM aliyepata kura 1,163. Kwa matokeo hayo, Chadema sasa kimefikisha madiwani 12 wakati CCM kimebakiwa na kumi na moja na TLP kina wawili.
Ushindi huo wa Chadema una athari kwa nafasi ya Meya wa Jiji la Arusha, Gaudence Lyimo kwani CCM kina wajumbe 14 tu kwenye Baraza la Madiwani, TLP wawili wakati Chadema sasa kimefikisha 15. Wabunge wa majimbo na wale wa viti maalumu pia ni madiwani.
Aidha, Chadema kina nafasi ya kuongeza kiti kingine cha udiwani kwani Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kinatarajiwa kuitisha uchaguzi mdogo Kata ya Sombetini.
Mkurugenzi wa NEC, Julius Malaba alimwambia mwandishi wetu kuwa tume yake inatarajia kuitisha uchaguzi mdogo hivi karibuni baada ya kata hiyo kutangazwa wazi na Ofisi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tamisemi.
Malaba alisema uchaguzi huo utaitishwa baada ya aliyekuwa Diwani wake, Alphonce Mawazo kujitoa CCM na kujiunga na Chadema hali inayokifanya chama tawala kuwa katika wakati mgumu kukitetea kiti hicho.
Wachache wajitokeza
Uchaguzi ulikuwa na idadi ndogo ya wapigakura kulinganisha na chaguzi zilizopita.
Elerai inayoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wapigakura 23,885 waliojitokeza ni 3,824 tu ikifuatiwa na Kimandolu yenye wapigakura 17,209 lakini waliopiga kura ni 3,967.
Kata ya Kaloleni ina wapigakura 12,674 hata hivyo, waliopiga kura ni 2,292. Themi yenye wapigakura wachache kuliko zote ikiwa na watu 6,387 lakini waliojitokeza kupiga kura ni 1,319 tu.
Licha ya idadi hiyo ndogo, baadhi ya wapigakura waliojitokeza walishindwa kutimiza dhamira yao baada ya kugundulika dosari kadhaa kwenye vitambulisho vyao na Daftari la Kudumu la Wapigakura.
“NEC wamevuruga uchaguzi huu makusudi kwa kuchezea Daftari la Wapigakura kwa nia ya kukibeba CCM. Haiwezekani waliopiga kura Uchaguzi Mkuu mwaka 2010 leo hii waambiwe majina yao hayamo kwenye daftari,” alilalamika mgombea udiwani Kata ya Kaloleni, Abbas Mkindi ‘Darweshi’.
Mkindi aliyewania kiti hicho kupitia CUF alitoa mfano wa mtoto wake, Omar Othman mwenye kitambulisho cha mpigakura namba 32479962 alichokitumia mwaka 2010 kuzuiwa kupiga kura baada ya jina lake kukosekana kwenye Daftari hilo. Wapiga kura wengine, Godchan Msella mwenye kadi namba 32479396  na Richard Minja mwenye namba 32479311 alizuiwa kupiga kura baada ya kubainika kuwa namba iliyopo kwenye Daftari ni tofauti na ya kadi yake.
Kutokana na kuwapo kwa mkanganyiko huo, Makamu Mwenyekiti wa NEC, Hamid Mohamoud Hamid alilazimika kuwaita wataalamu wa mfumo wa kompyuta (IT), katika Kituo cha Kupiga Kura cha Kaloleni kusaidia, kazi ambayo ilifanywa na timu iliyoongozwa na Seif Mtero.
Malaba alikiri uwezekano wa kutokea tofauti za tarakimu kwenye vitambulisho vya wapigakura na Daftari la Kudumu la Wapigakura huku akishauri wasimamizi na mawakala wa vyama kutumia busara kuruhusu wananchi wenye vitambulisho na maelezo sahihi kupiga kura.
“Tofauti ya tarakimu kwenye kadi ya mpigakura na Daftari la Mpiga Kura ni kosa la NEC, hivyo siyo sahihi kuwahukumu wapiga kura kwa kuwanyima haki yao ya kuchagua viongozi wawapendao,” alisema Malaba.
Amani yatawala
Ukiacha dosari na idadi ndogo ya wapiga kura, uchaguzi huo ulifanyika kwa amani na utulivu mkubwa tofauti na hofu iliyokuwapo awali kwamba huenda vurugu zingeibuka kutokana na mvutano uliopo kati ya vyama vya CCM na Chadema.
CHANZO: www.mwananchi.co.tz

Jumatatu, 1 Julai 2013

Rais Barack Obama awasili Tanzania

Rais wa Marekani Barack Obama, amewasili nchini Tanzania katika mkondo wake wa mwisho wa ziara yake barani Afrika.

Ziara ya Obama inasemekana kulenga kuimarisha uhusiano wa kibiashara na Afrika huku kukiwa na wasiwasi kuwa Marekani inaachwa nyuma na China katika uhusiano wao na Afrika. 

Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete na familia yake pamoja na maafisa wake wa serikali na wacheza densi za kitamaduni walimkaribisha Obama na familia yake mjini Dar es Salaam.

Obama amewasili Tanzania baada ya ziara yake ya Afrika Kusini ambako rais mstaafu Nelson Mandela anaugua.

Baadhi ya wananchi wa Tanzania kupitia mitandao ya kijamii wamekosoa ziara ya Obama katika nchi yao, wakisema kuwa ziara yake imeathiri shughuli za maisha yao ya kila siku.

Obama alitembelea Senegal kabla ya kupitia Afrika Kusini na kisha Tanzania ambako ziara yake ya Afrika inaishia kabla ya kurejea Marekani.

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More