Akilitz Technologies

Ni wataalama walio bobea katika Teknologia ya habari na mawasiliano ya Kompyuta na mitandao ya inteneti

This is default featured post 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Ijumaa, 30 Agosti 2013

MWANAJESHI WA UN AUAWA NCHINI DRC

Umoja wa Mataifa umesema kuwa mwanajeshi wake mmoja wa kutunza amani ameuawa na wengine watatu kujeruhiwa kufuatia mapigano makali kati ya na wapiganaji wa waasi Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa mjini New York, Farhan Haq, hata hivyo hajatangaza uraia wa wanajeshi waliouawa au kujeruhiwa.
Wanajeshi hao wa Umoja wa Mataifa walitumia ndege za helicopta kuwasukuma nyuma wapiganaji wa M23 karibu na mji wa Goma, ambao ndio mji mkubwa zaidi katika eneo hilo la Mashariki.
Watu themanini waliuawa kwenye mapigano hayo wiki iliyopita.
Mwaka wa 2012, waasi wa M23 waliuteka mji huo kwa muda kabla ya kuondoka kufuatia shinikizo kutoka kwa jamii ya kimataifa.
Umoja wa Mataifa Umetuma kikosi maalum katika eneo hilo lenya utajiri mkubwa wa madini kukabiliana na waasi hao.
Wanajeshi hao wa Umoja wa Mataifa MONUSCO, wanapambana na wapiganaji hao wa waasi kwa ushirikiano na wanajeshi wa serikali.

Silaha kali

Jeshi hilo la Monusco limelazimika kufanya mashambulio ya anga na ardhini ili kuzuia waasi hao wa M23 kukaribia Goma na ripoti zinasema mapigano makali yanaendelea katika maeneo ya milima ya Kibati, takriban kilomita kumi na tano Kaskazini mwa Goma.
Watu wapatano laki mbili wanasemekana kuishi katika eneo hilo la Kibati.
Wapiganaji wa M23 wamesema kuwa wanajeshi wa Congo na wenzao wa Umoja wa Mataifa walifanya mashambulio ya anga na ardhini katika maeneo wanayoyadhibiti, Kaskazini mwa Goma.
Daktarri mmoja mjini Goma, Isaac Warwanamiza, ameliambia shirika la habari la AP kuwa aliona miili ya watu themanini na wawili, ishirini na tatu zikiwa za wanajeshi wa serikali.
Umoja wa Mataifa una zaidi wanajeshi elfu kumi na nane nchini Congo

UINGEREZA INAWEZA KUISHAMBULIA SYRIA BILA IDHINA YA UN

Uingereza huenda ikaanzisha mashambulio dhidi ya utawala wa Syria, bila kuungwa mkono na Umoja wa Mataifa.
Hayo ni kwa mujibu wa ushauri wa wataalamu wake wa masuala ya kisheria.
Ushauri huo unasema, mashambulio hayo yatahitajika ikiwa yatatekelezwa ili kuzuia raia kuuawa, hata ikiwa wanachama wa kudumu wa baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Urussi na Uchina zikitumia kura zao za turufu kupinga mikakati za kijeshi dhidi ya utawala wa Syria.
Maafisa wa ujasusi nchini Uingereza wamemueleza Waziri Mkuu, David Cameron kuwa, kuna uwezekano mkubwa kuwa serikali ya Syria ilihusika na shambulio la kemikali wiki iliyopita mjini Damascus.
Wabunge wa Uingereza wanatarajiwa kujadili suala hilo katika kikao chao cha leo jioni.
Serikali ya Syria imekana madai ya kutumia silaha za kemikali katika shambulio mjini Damascus tarehe 21 mwezi huu, ambapo mamia ya watu waliuawa.
Lakini Bwana Cameron anaamini kuwa kuna ushahidi wa kutosha kutoka wa maafisa wake wa ujasusi na pia kutoka kwa wanainchi kuhusu ukatili unaofanywa na utawala wa sasa wa Syria.
Ofisi ya Waziri mkuu wa Uingereza, imechapisha ripoti hiyo, kuambatana na ushauri wa mkuu wake wa sheria Dominic Grieve, inayotoa idhini ya mashambulio ya kijeshi ili kuzuia utumiaji wa silaha za kemikali siku zijazo, kuambatana na sheria za kimataifa.

Umoja wa Mataifa

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon amesema atapokea ripoti kutoka kwa wachunguzi wake wa silaha, wanaochunguza ikiwa silaha za kemikali zilitumika nchini Syria.
Mamia ya watu wanaripotiwa kuuawa kwenye shambulio hilo, lililofanyika karibu na mji mkuu wa Damascus wiki iliyopita.
Rais wa Marekani Barack Obama, am
Mataifa mengine pia yanajadili hatua watakayo chukua na Uingereza imekuwa ikishinikiza baraza la Usalama la Usalama la Umoja wa Mataifa kuidhinisha azimio litakalihakisha raia wamelindwa nchini Syria.
Rais wa Syria Bashar al-Assad amesema taifa lake litajilinda kutokana na shambulio lolote kutoka kwa mataifa ya kigeni.

Syria kujilinda asema Assad

Awali Kiongozi wa chama cha Upinzani cha Labour, nchini Uingereza, Ed Miliband, amesema bunge la nchi hiyo halipaswi kuamua ikiwa itaidhinisha mzozo wa Syria kutatuliwa Kijeshi.
Milliband ameyasema hayo muda mfupi kabla ya bunge la Uingereza kupiga kura ikiwa Uingereza itaishambulia Syria, kufuatia madai ya kutumia silaha za kemikali mjini Damascus.
Waandishi wa habari wanasems serikali ya Uingereza inahofia huenda ikapoteza kura hiyo na hivyo kukosa idhini ya kuingilia mzozo huo wa Syria.
Milliband amesema wamejifunza mengi kutokana na maamuzi yaliyochukuliwa miaka ya zamani kama ule wa kuivamia Iraq.
Amesema jamii ya kimataifa inapaswa kuipa jopo maalum na wachunguzi wa Umoja wa Mataifa nafasi ya kufanya kazi yao.
Serikali ya Uingereza imesema ina habari za kujasusi kuhusu Syria na itachapisha ripoti hiyo na ushauri wa kisheria kabla ya mjadala huo kuanza bungeni.
esema ha
jaamua kuhusu mpango wa kuishambulia Syria kijeshi


 

Alhamisi, 22 Agosti 2013

Star wa "Prison Break" Wentworth Miller (MichaelScolfield) amejiweka wazi kuwa yeye ni Shoga

 
Star wa "Prison Break",  Wentworth Miller  a.k.a Michael Scofield, amejitangaza kuwa yeye ni "Gay" (shoga), katika barua ya wazi aliyoiandika kwenda kwa Directoe wa St. Petersburg International Film Festival (tamasha la filamu la kimataifa la St. Petersburg)

Muigizaji huyo (41) ameandika barua hiyo kukataa mualiko uliokuwa ukimtaka kuhudhuria tamasha hilo linalofanyika nchini kwao Russia na kwa mara ya kwanza kupitia barua hiyo amejitangaza kuwa yeye ni "Gay" (shoga).
"Asante kwa ukarimu wa mualiko wako, nikiwa kama mtu ambaye amefurahia kutembelea Russia kwa miaka ya nyuma na naweza pia kudai shahada ya asili ya kirusi, ningefurahi kusema ndio, hata hivyo nikiwa kama shoga lazima nikatae". amesema Miller

Miller akaendelea kusema ... nasumbuliwa sana na tabia ya sasa dhidi ya na jinsi wanavyochukuliwa mashoga na wanawake  na serikali ya Urusi.

"hali hii haikubaliki kabisa, na mimi siwezi kwa dhamira nzuri kushiriki katika tukio la kusherehekea linaloandaliwa (wenyeji) na nchi ambayo watu kama mimi kwa mfumo uliopo wananyimwa haki zao za msingi za kuishi na kupenda kwa uwazi"

akamalizia kwa kusema.. kama hali hii itarekebishwa, nitakuwa huru kufanya uchaguzi tofauti.

Alhamisi, 8 Agosti 2013

Bilionea Wama dini Mererani auawa kwa risasi 20 Moshi







Moshi. Mfanyabiashara tajiri wa Mirerani na Jijini Arusha, Erasto Msuya, ameuawa kwa kupigwa risasi zaidi ya 20 kwa kutumia bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG), jana mchana.
Erasto anayemiliki vitega uchumi kadhaa na anayeaminika kuwa miongoni mwa wafanyabiashara wa Mirerani wanaoongoza kwa utajiri,
aliuawa jana saa 7:00 mchana wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.
“Eneo la tukio kumeokotwa maganda karibu 21 ya risasi zinazoaminika ni za SMG, yaani mwili ni matobo kila sehemu kwa kweli ameuawa kinyama sana,” alisema polisi mmoja wa Kituo cha Bomang’ombe.
Kufuatia mauaji hayo yaliyotokea kati ya neo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) na mji wa Bomang’ombe, mji huo ulifurika magari ya wachimbaji kutoka Moshi, Arusha na Mererani.
Habari za uhakika zilieleza kuwa wauaji wake walikuwa katika pikipiki na baada ya kumminia risasi hizo, walimpora kibegi ambacho haikujulikana kama kilikuwa na madini ama mamilioni ya fedha.
Kulingana na vyanzo vya habari, mfanyabiashara huyo alipigiwa simu na kukubaliana kukutana katikati ya mji wa Bomang’ombe na makutano ya Barabara ya Kia katika Barabara Kuu ya Hai kwenda Arusha.
RPC Kilimanjaro afafanua alivyouawa
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema kuwa mfanyabiashara huyo aliuawa saa 7:00 mchana eneo la Mjohoroni kati ya mji wa Bomang’ombe na makutano ya barabara ya Kia.
“Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa Eransto alikuwa akitokea Moshi kuelekea Arusha, na alipofika hilo eneo la Mjohoroni alichepuka na kwenda meta 300 nje ya barabara,” alisema.
Kamanda Boaz alisema alipofika eneo hilo, alikutana na vijana wawili waliokuwa na pikipiki ambao waliingia ndani ya gari kwa lengo la kufanya mazungumzo yanayodhaniwa ni ya kibiashara.
Hata hivyo, muda mfupi tu Erasto alishuka kwenye gari lake na kuanza kukimbia na ndipo mmoja kati ya wale vijana alishuka kwenye gari la Erasto na kuanza kumminia risasi nyingi.
Kijana pekee wa kabila la kimasai anayedaiwa kushuhudia mauaji hayo, aliwaeleza polisi kuwa mara baada ya Erasto kufika eneo hilo la mtaa wa Wasomali, alisimamisha gari na kuwapigia wauaji.
Habari hizo zimedai kuwa vijana wale wawili walipokea simu hiyo na kumtaka ashuke kwenye gari lake la kifahari aina ya Range Rover New Model, ili wafanye biashara ambayo haijui.
Inadaiwa kuwa Erasto alipojaribu kupeleka mkono ili achomoe bastola, mmoja wa wale vijana alianza kumshambulia kwa risasi nyingi ambazo zilimfanya afariki dunia papo hapo.
Kijana huyo wa kimasai anayedaiwa kuwa msaada mkubwa kwa polisi, alidai kuwa baada ya Erasto kudondoka chini, vijana hao walichukua begi alilokuwa nalo na kutokomea.
Pikipiki iliyotumika yapatikana
Taarifa zilizopatikana baadaye jana jioni zilisema pikipiki iliyotumika katika tukio hilo imepatikana katika kijiji cha Olkolili, huko Sanyajuu wilayani Siha mkoani Kilimanjaro.
Kamanda Boaz alithibitisha kupatikana kwa pikipiki hiyo yenye nambari za usajili T316 CLV ikiwa imetelekezwa baada ya gurudumu moja kupata pancha baada ya kufika katika eneo hilo.
“Kwa vile tulikuwa tumesambaza taarifa kila mahali kwamba kuna raia wema walituarifu kuwa kuna watu wametelekeza pikipiki, baada ya kupata pancha na walikuwa wakitembea kwa miguu,” alisema.
Alisema Polisi walikwenda katika eneo hilo na mashuhuda walioshuhudia tukio hilo la mauaji wameitambua pikipiki hiyo kuwa ndiyo iliyokuwa ikitumiwa na wauaji wa mfanyabiashara huyo.
Kamanda Boaz alisema pia kuwa polisi watachunguza kwa kina mawasiliano ya simu ya mfanyabiashara huyo, kwa lengo la kutafuta watu wa mwisho kuwasiliana na marehemu.

Utajiri wake marehemu Msuya Katika kipindi cha uhai wake, marehemu alikuwa akijihusisha na uchimbaji na biashara ya madini ya Tanzanite katika mji mdogo wa Mirerani na jiji la Arusha. Kutokana na biashara zake hizo, alimudu kumiliki mali kadhaa zikiwemo nyumba za kawaida za kuishi pamoja na hoteli maarufu Arusha ya SG Resort iliyoko eneo la Sakina. Pamoja na hoteli na nyumba kadhaa zilizoko mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro, marehemu pia alikuwa akimiliki magari kadhaa ya kifahari. Nyongeza na Peter Saramba, Arusha

Ijumaa, 2 Agosti 2013

SAYANSI YA UFUFUAJI: MIAKA 20 IJAYO MADAKTARI WATAKUWA NA UWEZO WA KUWARUDISHIA UHAI WAGONJWA WALIOKATA ROHO!


dr
Twende taratibu, hii ni taarifa ya kisayansi na sio ‘kiimani’ na imetolewa na daktari bingwa wa moyo wa Marekani. Sasa naomba uniruhusu nikuelezee nilichokutana nacho kuhusiana na habari hii.
Dr Sam Parnia wa Marekani amedai kwamba kwa kupitia mbinu za kisasa za kitaalamu (kisayansi) kuna uwezekano wa kumrudishia uhai mgonjwa aliyekata roho ndani ya saa 24!! (hata mimi nimeguna)
Dr huyo wa moyo ambaye amepata mafunzo yake nchini Uingereza, ameendelea kusema hivi karibuni wanategemea kuanza kuokoa maisha ya wagonjwa wanaokuwa tayari wamekata roho katika masaa ya mwanzo baada ya kuthibitisha wamefariki. “We may soon be rescuing people from death’s clutches hours, or even longer, after they have actually died.” Alisema Dr Sam
Parnia ameendelea kutetea kauli hiyo kwa kusema kuwa muigizaji wa Marekani James Gandolfini aliyefariki mwezi uliopita angeweza kupona endapo angekuwa ameugulia tatizo lake la moyo New York.
“I believe if he died here, he could still be alive. We’d cool him down, pump oxygen to the tissues, which prevents them from dying, Clinically dead, he could then be cared for by the cardiologist. He would make an angiogram, find the clot, take it out, put in a stent and we would restart the heart,” Dr Parnia alilieleza jarida la Der Spiegel la Ujerumani.



dr-3
Dr Parnia ambaye ni mkuu wa kitengo cha ‘Intensive care’ katika hospitali ya the Stony Brook University iliyoko New York, Marekani aliendelea kusema ni kweli hawawezi kuokoa maisha ya kila mtu sababu wagonjwa wengi wa moyo huwa na matatizo mengine ya ziada na makubwa zaidi.
Aliendelea kusema kama teknolojia ya kisasa ya tiba na mafunzo vingekuwa vinafanyiwa kazi inavyotakiwa, (kitu ambacho anadai bado hakijafanyika) basi watu ambao wangetakiwa kufa ni wale tu wenye matatizo ambayo hayatibiki kabisa lakini sio ugonjwa wa moyo unaotibika.
’‘A heart attack is treatable. Blood loss as well. A terminal cancer isn’t, neither are many infections with multiresistant pathogens. In these cases, even if we’d restart the heart, it would stop again and again”.
Akielezea jinsi ambavyo mgonjwa wa moyo aliyefariki anavyoweza kurudishiwa uhai, alisema kwanza ni kuugandisha mwili mara tu baada ya kuthibitishwa amefariki , “freezing the body immediately after death – but cooling it down to best preserve brain cells while keeping up the level of oxygen in the blood. This buys time to fix the underlying problem and restart the heart”. Alisema
Dr huyo alisema kuna uwezekano katika miaka 20 ijayo madaktari watakuwa na uwezo wa kurudisha uhai wa wagonjwa masaa 12 hadi 24 toka wathibitishwe kufa na kuiita hiyo kuwa ni sayansi ya ufufuaji, “You could call that resurrection, if you will. But I still call it resuscitation science”.
Dr Parnia ameandika kitabu kipya kiitwacho ‘Erasing Death’.

SOURCE: DAILY MAIL

Jumatatu, 15 Julai 2013

CCM Chali, Chadema yaibuka kidedea Arusha

Chadema kimethibitisha umwamba wake katika siasa za Jimbo la Arusha Mjini, baada ya kutetea kwa kishindo kata zake nne kwenye uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika jana.
Katika uchaguzi huo uliokuwa unasubiriwa kwa hamu na ambao ulichukuliwa kama kipimo cha siasa za Arusha ambazo zimekuwa na mvutano mkubwa, Chadema kiliongoza katikia vituo vyote 136 vya kupigia kura Kata za Elerai, Kaloleni, Kimandolu na Themi.
Kata hizo zilikuwa wazi tangu mwaka 2011 baada ya Chadema kuwatimua wanachama wake waliokuwa madiwani Estomih Mallah(Kimandolu), John Bayo (Elerai), Reuben Ngowi (Themi) na Charles Mpanda (Kaloleni).
Matokeo
Katika matokeo yaliyotangazwa na Msimamizi wa Uchaguzi Kata ya Elerai, Obedi Meng’oriki mshindi alikuwa Jeremiah Mpinga wa Chadema aliyepata kura 2,047 dhidi ya 1,471 za Emmanuel Laizer wa CCM. Katika Kata hiyo kulikuwa na wagombea wengine ambao ni John Bayo (CUF; kura 302), Seif Shimba (CCK; kura 3) na Boisafi Shirima (TLP;1).
Katika Kata ya Themi, Kinabo Edmund wa Chadema aliibuka na ushindi baada ya kupata kura kupata kura 674. Msimamizi wa Uchaguzi Kata hiyo, Ezeka Mboya alisema Kinabo alifuatiwa na Victor Mkolwe aliyepata kura 326 na Lobora Ndarpoi wa CUF alipata kura 307.
Kata ya Kaloleni, Msimamizi wa Uchaguzi, Anna Ledisa alimtangaza Kessi Lewi wa Chadema kuwa mshindi kwa kura 1,470 dhidi ya Emmanuel Mliari wa CCM aliyepata kura 330 na Abbas Mkindi wa CUF aliyepata kura 275 na Ngilishi Pauli wa Demokrasia Makini aliyeambulia kura mbili.
Kata ya Kimandolu, Msimamizi wa Uchaguzi, Suleiman Kilingo alimtangaza Mchungaji Rayson Ngowi wa Chadema kuwa mshindi kwa kura 2,761 na kumshinda Edna Saul wa CCM aliyepata kura 1,163. Kwa matokeo hayo, Chadema sasa kimefikisha madiwani 12 wakati CCM kimebakiwa na kumi na moja na TLP kina wawili.
Ushindi huo wa Chadema una athari kwa nafasi ya Meya wa Jiji la Arusha, Gaudence Lyimo kwani CCM kina wajumbe 14 tu kwenye Baraza la Madiwani, TLP wawili wakati Chadema sasa kimefikisha 15. Wabunge wa majimbo na wale wa viti maalumu pia ni madiwani.
Aidha, Chadema kina nafasi ya kuongeza kiti kingine cha udiwani kwani Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kinatarajiwa kuitisha uchaguzi mdogo Kata ya Sombetini.
Mkurugenzi wa NEC, Julius Malaba alimwambia mwandishi wetu kuwa tume yake inatarajia kuitisha uchaguzi mdogo hivi karibuni baada ya kata hiyo kutangazwa wazi na Ofisi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tamisemi.
Malaba alisema uchaguzi huo utaitishwa baada ya aliyekuwa Diwani wake, Alphonce Mawazo kujitoa CCM na kujiunga na Chadema hali inayokifanya chama tawala kuwa katika wakati mgumu kukitetea kiti hicho.
Wachache wajitokeza
Uchaguzi ulikuwa na idadi ndogo ya wapigakura kulinganisha na chaguzi zilizopita.
Elerai inayoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wapigakura 23,885 waliojitokeza ni 3,824 tu ikifuatiwa na Kimandolu yenye wapigakura 17,209 lakini waliopiga kura ni 3,967.
Kata ya Kaloleni ina wapigakura 12,674 hata hivyo, waliopiga kura ni 2,292. Themi yenye wapigakura wachache kuliko zote ikiwa na watu 6,387 lakini waliojitokeza kupiga kura ni 1,319 tu.
Licha ya idadi hiyo ndogo, baadhi ya wapigakura waliojitokeza walishindwa kutimiza dhamira yao baada ya kugundulika dosari kadhaa kwenye vitambulisho vyao na Daftari la Kudumu la Wapigakura.
“NEC wamevuruga uchaguzi huu makusudi kwa kuchezea Daftari la Wapigakura kwa nia ya kukibeba CCM. Haiwezekani waliopiga kura Uchaguzi Mkuu mwaka 2010 leo hii waambiwe majina yao hayamo kwenye daftari,” alilalamika mgombea udiwani Kata ya Kaloleni, Abbas Mkindi ‘Darweshi’.
Mkindi aliyewania kiti hicho kupitia CUF alitoa mfano wa mtoto wake, Omar Othman mwenye kitambulisho cha mpigakura namba 32479962 alichokitumia mwaka 2010 kuzuiwa kupiga kura baada ya jina lake kukosekana kwenye Daftari hilo. Wapiga kura wengine, Godchan Msella mwenye kadi namba 32479396  na Richard Minja mwenye namba 32479311 alizuiwa kupiga kura baada ya kubainika kuwa namba iliyopo kwenye Daftari ni tofauti na ya kadi yake.
Kutokana na kuwapo kwa mkanganyiko huo, Makamu Mwenyekiti wa NEC, Hamid Mohamoud Hamid alilazimika kuwaita wataalamu wa mfumo wa kompyuta (IT), katika Kituo cha Kupiga Kura cha Kaloleni kusaidia, kazi ambayo ilifanywa na timu iliyoongozwa na Seif Mtero.
Malaba alikiri uwezekano wa kutokea tofauti za tarakimu kwenye vitambulisho vya wapigakura na Daftari la Kudumu la Wapigakura huku akishauri wasimamizi na mawakala wa vyama kutumia busara kuruhusu wananchi wenye vitambulisho na maelezo sahihi kupiga kura.
“Tofauti ya tarakimu kwenye kadi ya mpigakura na Daftari la Mpiga Kura ni kosa la NEC, hivyo siyo sahihi kuwahukumu wapiga kura kwa kuwanyima haki yao ya kuchagua viongozi wawapendao,” alisema Malaba.
Amani yatawala
Ukiacha dosari na idadi ndogo ya wapiga kura, uchaguzi huo ulifanyika kwa amani na utulivu mkubwa tofauti na hofu iliyokuwapo awali kwamba huenda vurugu zingeibuka kutokana na mvutano uliopo kati ya vyama vya CCM na Chadema.
CHANZO: www.mwananchi.co.tz

Jumatatu, 1 Julai 2013

Rais Barack Obama awasili Tanzania

Rais wa Marekani Barack Obama, amewasili nchini Tanzania katika mkondo wake wa mwisho wa ziara yake barani Afrika.

Ziara ya Obama inasemekana kulenga kuimarisha uhusiano wa kibiashara na Afrika huku kukiwa na wasiwasi kuwa Marekani inaachwa nyuma na China katika uhusiano wao na Afrika. 

Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete na familia yake pamoja na maafisa wake wa serikali na wacheza densi za kitamaduni walimkaribisha Obama na familia yake mjini Dar es Salaam.

Obama amewasili Tanzania baada ya ziara yake ya Afrika Kusini ambako rais mstaafu Nelson Mandela anaugua.

Baadhi ya wananchi wa Tanzania kupitia mitandao ya kijamii wamekosoa ziara ya Obama katika nchi yao, wakisema kuwa ziara yake imeathiri shughuli za maisha yao ya kila siku.

Obama alitembelea Senegal kabla ya kupitia Afrika Kusini na kisha Tanzania ambako ziara yake ya Afrika inaishia kabla ya kurejea Marekani.

Jumatatu, 24 Juni 2013

Brazil yazidi kusonga mbele Kombe la Mabara


Mshambuliaji wa Italia, Mario Balotelli (kushoto) akizuiwa na beki wa Brazil, David Luiz wakati wa mechi ya Mabara kwenye Uwanja wa Fonte Nova mjini Salvador. Picha AFP.  

Brazil. Timu ya taifa ya Brazil juzi imeichapa Italia 4-2 katika mashindano ya Kombe la Mabara na hivyo Brazil kumaliza hatua ya makundi ikiongoza kundi A.
Mshambuliaji Neymar wa Brazil katika mechi hiyo alifunga bao na hivyo kufikisha mabao matatu katika mashindano hayo.
Brazil ilipata bao la kwanza mwishoni mwa kipindi cha kwanza ambalo lilifungwa na Dante, lakini Italia ilisawazisha bao hilo katika dakika ya 51 mfungaji akiwa Emanuele Giaccherini.
Katika dakika ya 55, Neymar aliifungia Brazil bao la pili baada ya kupiga mpira wa adhabu uliokwenda moja kwa moja nyavuni na kumuacha kipa mahiri wa Italia, Gianluigi Buffon asijue la kufanya.
kama hiyo haitoshi Brazil ilipata bao la tatu katika dakika ya 66 ambalo lilifungwa na Fred, lakini Italia nao hawakubaki nyuma kwani katika dakika 71 walifunga bao la pili ambalo lilifungwa na Giorgio Chiellini.
Katika dakika ya 80 bado kidogo Italia wangesawazisha hata hivyo mpira wa kichwa uliopigwa na Christian Maggio ulipita juu kidogo ya goli. Pia dakika chache baadaye Mario Balotelli naye alipiga shuti kali, lakini lilitoka nje.
Ilipofika dakika ya 89, Brazil ilijihakikishia ushindi wa mechi hiyo kwani Fred alitumia vizuri mpira uliopanguliwa na kipa wa Italia na hivyo kuiandikia Brazil bao la nne.
Brazil imemamaliza hatua hii ya makundi ikiwa na pointi tisa ikiwa na pointi tatu juu ya Italia inayomfuatia huku timu za Mexico na Japan zikitolewa mashindanoni.
“Brazil ipo tayari kwa ajili ya mechi ya nusu fainali, tumefanikiwa kusonga mbele kwa sababu ya ufundi mzuri na mbinu bora, pia kikosi kinajiamini,”alisema kocha wa Brazil, Luiz Felipe Scolari.

Jumapili, 23 Juni 2013

Vigogo wahaha - wahojiwa mabilioni ya Uswis

Dar es Salaam. Suala la baadhi ya Watanzania kuhifadhi mabilioni ya fedha nchini Uswisi limechukua sura mpya, baada ya tume maalumu kuwahoji vigogo 200 wakiwamo wabunge, wanasiasa na wafanyabiashara.
Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa tume hiyo inayoongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema tayari imeshafanya kazi hiyo kwa miezi miwili sasa.
Tume hiyo maalumu iliyoundwa na Serikali kwa Azimio la Bunge lililotolewa mwishoni mwa mwaka jana, inatarajiwa kukamilisha uchunguzi huo wakati wowote kuanzia sasa na kuwasilisha ripoti hiyo katika kikao kijacho cha Bunge. Jaji Werema alipoulizwa na Mwananchi Jumpili maendeleo ya uchunguzi huo, alisema kuwa kazi hiyo bado inaendelea.
“Uchunguzi huo unaendelea,” alisema Werema huku akisita kueleza kwa undani juu ya kazi hiyo kwa kile alichosema kuwa hana sababu ya kufanya hivyo kwa sasa.
“Subiri uchunguzi bado unafanywa,” alisema Werema na alipotakiwa kueleza utamalizika lini alisema: “Utamalizika tu.”
Mwanasheria huyo wa Serikali alikataa kutaja baadhi ya majina ya watu ambao tume yake imewahoji mpaka sasa.
Alisema anashangazwa na swali la namna hiyo, kwa maelezo kwamba ni jambo ambalo liko wazi kuwa ni kinyume na maadili kuwataja watuhumiwa wakati huu uchunguzi ukiwa bado unaendelea.
Uchunguzi huo unafanyika baada ya Benki ya Taifa ya Uswiss (SNB) kutoa taarifa mwezi Juni, 2012 kuhusu raia wa kigeni wanaomiliki akaunti za benki nchini humo.
Orodha hiyo iliorodhesha pia baadhi ya Watanzania wenye akaunti zinazofikia Dola196 milioni ambazo ni sawa na Sh323.4 bilioni.
Jarida la kimataifa la uchunguzi la The Indian Ocean Newsletter toleo la hivi karibuni, lilimnukuu Werema akisema uchunguzi huo kwa sasa unatia matumaini.
Werema anaripotiwa akiri kuwa uchunguzi huo umefikia ‘hatua ya kutia matumaini’ na wanaendelea na kazi hiyo kwa uangalifu ili kuwa na uhakika wa taarifa wanazozitafuta.
Alisema kwamba taarifa ya awali inatarajiwa kutolewa hivi karibuni na tayari idadi kubwa ya wahusika wakiwamo wabunge wameshahojiwa.
Werema alisema wanaendelea na uchunguzi kuwabaini zaidi ya Watanzania 200, waliotajwa kuficha mabilioni ya fedha nje ya nchi.
Mbali na Werema, tume hiyo inaundwa na viongozi kadhaa wa taasisi nyeti kama vile Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hosea, Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Rashid Othman na Gavana wa Benki Kuu (BoT), Profesa Benno Ndulu.
Tume hiyo inawahusisha pia Mkuu wa Sheria wa BoT, Mustapha Ismail na maofisa kutoka idara ya upelelezi na ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali.
Kwa mujibu wa jarida hilo la kimataifa, miongoni mwa watuhumiwa hao ni wanasiasa na majenerali wastaafu wanaotuhumiwa kutorosha zaidi ya Dola 133 milioni mwaka 2005, kupitia Mfuko wa Ulipaji Madeni ya Nje (EPA)
Baadhi ya watu wanaodaiwa kuhusika wamehojiwa kutokana na taaluma zao, familia zao, akaunti zao za benki zilizoko nchini na nje ya nchi pamoja na nchi walizotembelea mara kwa mara kwa miaka mitatu iliyopita.
Lengo la kuwahoji inaelezwa ni kutaka kujua iwapo walifuata njia zinazotakiwa katika kufungua akaunti hizo nje ya nchi na iwapo fedha zilizohifadhiwa huko zilipatikana kihalali.
Sakata la kashfa hiyo liliibuliwa Bungeni kwa hoja binafsi ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe mwishoni mwa mwaka 2012.
Zitto alisema kwamba kiasi cha fedha kilichofichwa nchini Uswisi ni kikubwa zaidi ya hicho kilichotajwa.
Bunge liliipa Serikali kipindi cha mwaka mmoja ambacho kinaishia Oktoba mwaka huu, iwe imekamilisha uchunguzi na kuwasilisha ripoti hiyo bungeni.

Jumanne, 18 Juni 2013

Tizama matukio mbali mbali ya chama cha CHADEMA wakiwafariji wafiwa na majeruhi baada ya Mlipuko wa Bomu


Mwenyekiti wa Chadema, Mh Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema wakiwa nyumbani kwa wazazi wa mmoja wa marehemu (Ramadhani) eneo la Mianzini kuwapa pole kwa kuondokewa na mpendwa wao.




Eneo la maafa. Inaelezwa kuwa wataalamu wa jeshi waligundua kuwako kwa kitu ndani yatanki la mafuta na hivyo kuamua kulikata. Taarifa hizo zinadai kwamba kulikuwa na mabomu yametegwa chini ya gari na hivyo tanki hilo lilishambuliwa kwa risasi labda utokee mlipuko! Pia gari hii ya matangazo lina majeraha mawili mlango wa kushoto yaliyotokana na kitu chenye ncha ambacho kinaweza kuwa risasi au vipande vya vyuma vya bomu.



Dereva wa mgombea wa Chadema Kata ya Themi, Bwana Benny akiwa hospitali


James Ole Millya na Mbunge Lema wakimjulia hali mmoja wa majeruhi walilazwa hospitali ya Seliani.

Jumatano, 12 Juni 2013

TFDA: Kiwanda cha TPI kilisambaza ARV feki kwa Watanzania


MAMLAKA ya Chakula na Dawa (TFDA), imethibitisha dawa bandia za kupunguza makali ya Virusi Vya Ukimwi (ARV), zilitengenezwa na kiwanda cha Tanzania Pharmaceutical Industry (TPI). Taarifa hiyo, ilitolewa jana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Hiiti Sillo, wakati wa semina kwa wabunge iliyoandaliwa na Bohari ya Dawa (MSD).

Sillo, alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali (NCCR-Mageuzi), aliyetaka kujua kama dawa hizo bandia za ARV kweli zilitengenezwa na kiwanda cha TPI.

“Ninyi TFDA, mlikuwa wapi hadi kiwanda hicho kinazalisha dawa bandia za ARV?” alihoji Machali.

Alisema ni kweli dawa hizo bandia, ziligundulika zikiwa tarari zipo sokoni katika hospitali mbalimbali, ikiwemo Hospitali ya Tarime mkoani Mara.

“TDFA ilifanya uchunguzi wa kitaalamu na kubaini dawa hizo ni bandia na baada ya uchunguzi pia na kwa mujibu wa nyaraka, ilibainika dawa hizo zilitengenezwa na Kiwanda cha TPI ambayo ndiyo iliyoisambazia dawa hizo MSD,” alisema Sillo.

Mbunge wa Njombe Kaskazini, Deo Sanga (CCM), aliitaka Serikali kupeleka muswada bungeni kutunga sheria kali kwa watakaobainika kuuza dawa za Serikali katika maduka binafsi.

“Sheria hii kali ikitungwa, dawa za Serikali hazitakutwa kwenye maduka binafsi na zikikutwa zitaifishwe,” alisema.

Awali akifungua semina hiyo, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi, alisema lengo la semina hiyo ni kushirikishana uzoefu na wabunge juu ya mfumo wa usambazaji dawa nchini.

Alisema semina hiyo, ilikuwa na mada nne, ikiwemo hiyo ya mfumo wa usambazaji wa dawa na vifaa tiba wa Bohari ya Dawa, ikiwemo kuzungumzia mikakati mbalimbali ya kuongeza ufanisi katika upatikanaji wa dawa katika vituo vya kutolea huduma.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa MSD, Cosmas Mwaifwani, alisema mbali na jitihada mbalimbali zinazofanywa na bohari hiyo, aliwaomba wateja wake kuboresha mfumo wa utunzaji kumbukumbuku katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya katika ngazi zote.

“Kuongeza usimamizi wa dawa na vifaa tiba ngazi ya wilaya, kupitia Kamati za Afya za Wilaya ili kuboresha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba vituoni,” alisema.

Messi na babake wadaiwa kulaghai serikali


Mshambulizi matata wa Barcelona Lionel Messi na babake wanachunguzwa nchini Uhispania kwa kuilaghai serikali ya nchi hiyo zaidi ya pauni milioni tatu nukta nne.
Mchezaji huyo kutoka Argentina na babake, Jorge wanatuhumiwa kuibia serikali ya nchi hiyo, kwa kujaza fomu zizizokuwa za ukweli za marejesho ya kodi kati ya mwaka wa 2007 na 2009.
Hata hivyo mechezaji huyo mwenye umri wa miaka ishirini na mitano hajasema lolote kuhusiana na madai hayo.
Messi hulipwa Euro milioni kumi na sita kila mwaka na ndiye mchezaji anayelipwa kiasi cha juu zaidi duniani.
Lakini mwendesha mashtaka Raquel Amado, aliwasilisha nyaraka za mahakama nyumbani kwake kwa mchezaji huyo katika mtaa wa kifahari wa Gava mjini Barcelona.
Jaji mjini humo ni sharti waidhinisha malalamishi dhidi ya mshukiwa yeyote kabla hajafunguliwa mashtaka.
Messi na babake wanashukiwa kutumia kampuni katika mataifa ya ngambo, mjini Belize na Uruguay kuuza haki za kutumia picha ya mchezaji huyo.
Mchezaji huyo na babake wanatuhumiwa kutumia kampuni hizo zilizoko nje ya Uhispania, ambako anaishi na kucheza soka ya kulipwa, kukwepa kulipa kodi inayokisiwa kuwa pauni milioni tatu na nusu.

CHANZO: bbc.co.uk/swahili

Alhamisi, 6 Juni 2013

MTOTO WA MICHAEL JACKSON ATAKA KUJIUA





Imeripotiwa kuwa mtoto wa marehemu Michael jackson,Paris Jackson  amekimbizwa hospitalin
baada ya kufanya jaribio la kujiuwa. Jackson Paris  mwenye umri wa miaka 15 sasa,alikimbizwa hospitali mapema Jumatano asubuhi na vyanzo kutuambia ilikuwa jaribio kujiua.Ripoti inasema kuwa alijiovadozi kwa dawa ambazo bado hazijafahamika Ndugu wa karibu na Paris jackson  wameuambia mtandao wa TMZ toka America kuwa hiyo yawezakuwa si jaribio la kwanza  kwani ana alama za  kujichanja kwa kifaa chenye ncha kali kwenye mkono wake.Siku moja kabla ya tukio hilo,Paris jackson alitweet maneno yafuatayo yenye mafumbo: “I wonder why tears are salty?” … na “yesterday, all my troubles seemed so far away now  it looks as though they’re here to stay.”





BREAKING NEWS: MUME WA KHADIJA KOPA AFARIKI DUNIA



                              Khadija Omar Kopa akiwa na mumewe Jaffari Ally enzi za uhai wake


Mume wa Malkia wa Mipasho Afrika Mashariki, Khadija Omar Kopa, aitwaye Jaffari Ally amefariki dunia usiku wa kuamkia leo. Marehemu alikuwa anasumbuliwa na matatizo katika mfumo wa upumuaji na mpaka mauti yanamfika alikuwa amelazwa katika hospitali ya Lugalo jijini Dar es Salaam.

Jumanne, 4 Juni 2013

KIBANDA AREJEA KUTOKA AFRIKA KUSINI, KWA KISHINDO


                                  Kibanda akiongea na waandishi wa habari alipowasili air port

                                       Hapa akilia kwa uchungu baada ya kuwasili airport


BAADA ya kuwa Afrika Kusini  majuma kadhaa kwa ajili ya matibabu, Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya New Habari 2006 na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda, hatimaye  amerejea nyumbani leo mchana na  kulakiwa na mamia ya waandishi wa habari.

Tizama picha zinazoonyesha kuwasili kwa mwili wa Albert Mangwea


Wasanii,waandaji,mashabiki na wadau wa muziki wa kizazi kipya Tanzania wameungana kupokea mwili wa marehemu Albert Mangwear pale Air Port Mchana wa leo.Albrt Mangweha "Ngwair" alifariki Jumanne iliyopita 28/5/2013 huko Afrika Kusini
 

Mwili wa marehemu Albert Mangweha a.k.a Ngawair ukiwa unapakiwa kupelekwa Airport kwa ajili ya kuletwa Tanzania.…

Jumatatu, 3 Juni 2013

Maandamano yakutaka kumngoa JK yanaandaliwa


MAANDAMANO makubwa ya kutaka Rais Jakaya Kikwete asikilize kilio cha wakazi wa Mtwara na Lindi wanaopinga ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam yanaandaliwa.
Baadhi ya wakazi wa Lindi na Mtwara kwa kushirikiana na Chama cha Wananchi (CUF), Juni 29 mwaka huu wanatarajia kufanya maandamano hayo kutoka makao makuu ya CUF Buguruni hadi Ikulu, jijini Dar es Salaam.
Maandamano hayo pia yatakuwa na lengo la kumtaka Rais Kikwete awang’oe madarakani mawaziri watatu ambao ni Profesa Sospeter Muhongo (Nishati na Madini), Shamsi Vuai Nahodha (Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa), Emanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani).
Wakizungumza katika mkutano wa kongamano la gesi lililowakutanisha wakazi wa Lindi na Mtwara, lililofanyika jana jijini Dar es salaam katika Ofisi za Makao Makuu ya CUF, baadhi ya wakazi hao walisema wamechoshwa na ahadi za serikali.
Walisema wanaamua kufanya maandamano kwenda Ikulu ili kilio chao kimfikie Rais Kikwete ambaye kama hatakisikiliza asitarajie wananchi watarudi nyuma kutetea rasilimali zilizoko mikoani mwao.
Walibainisha kuwa vurugu zilizotokea hivi karibuni mkoani Mtwara ni ishara ya kuchoshwa na mgawanyo wa rasilimali unaofanywa na serikali ambayo hivi sasa badala ya kuufikiria mkoa wa Mtwara unahangaika kujenga bomba la gesi kutoka mkoani humo.
Lipumba aanza
Akifungua mkutano huo, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba, alisema vurugu zilizotokea hivi karibuni mkoani Mtwara zimesababishwa na serikali ya CCM iliyopuuza kilio cha umaskini cha wakazi cha mkoa huo.
Alisema serikali imeanza kushtuka na kwenda kuweka msingi wa ujenzi wa kiwanda cha saruji baada ya machafuko na upinzani kutoka kwa wananchi.
Alibainisha kuwa nguvu na kuwaziba midomo wanasiasa, wananchi na wanaharakati kamwe hazitoisaidia serikali kutatua mzozo huo unaoonekana kuutikisa utawala wa Rais Kikwete.
Aliongeza kuwa watu wa Mtwara na Lindi wamekosa mahali na fursa za kuonana na viongozi wao kuzungumzia suala la gesi na matokeo yake imesababisha vurugu, manyanyaso kutoka kwa polisi waliokwenda kutuliza ghasia.
Profesa Lipumba alisema serikali inaeneza propaganda za uongo kwamba wananchi wa Mtwara hawataki Watanzania wengine wafaidi rasilimali zinazotoka katika mkoa huo.
Alisema wananchi wanataka maendeleo yaanzie katika mkoa huo kutokana na rasilimali zilizopo ndani yake ikiwemo kujengwa kiwanda cha mbolea na kiwanda cha kufua umeme wa MW 300 kama ahadi ya serikali ya mwaka 2011 inavyoeleza.
Aliongeza kuwa serikali katika ahadi zake miaka miwili iliyopita iliwaeleza wananchi wa Mtwara kwamba ingejenga kiwanda cha mbolea na kujenga kiwanda cha kufua gesi ambayo ingezalisha umeme wa MW 300 kisha uunganishwe kwenye gridi ya taifa lakini mipango hiyo haikufanyika.
Alisisitiza kwamba endapo mipango ya serikali iliyoainishwa kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ingetekelezwa hakuna vurugu wala matatizo ambayo yangejitokeza.
Alisema wananchi wanaoishi mikoa ya kusini wanadharaulika na kuonekana hawastahili kupata haki kama watu wa mikoa mingine na kwamba hali hiyo imewafanya wachoke na kufanya matendo ambayo yataaonyesha kuchoshwa na kuhitaji mabadiliko.
Wakazi wafunguka
Baada ya Lipumba kuzungumza, wakazi waliokuwapo ukumbini hapo walipata fursa ya kutoa dukuduku ambapo wengi wao walitaka mawaziri watatu wang’olewe madarakani.
Waziri Nchimbi anatakiwa kung’olewa kwa sababu ya kutowachukulia hatua polisi waliokwenda kutuliza ghasia mkoani humo kuendesha vitendo vya kihalifu, kubaka na kuwanyanyasa wananchi.
Mmoja wa wakazi hao alisema Nchimbi alisema damu ya polisi iliyomwagika haitapotea bure wakati askari hao walikufa kwenye ajali wakiwa njiani kwenda Mtwara.
“Polisi hawakufa kwenye mapambano, walikufa kwa ajali ya gari lao sasa wananchi watalipa vipi vifo hivyo? Waziri Nchimbi alichemka na hatufai,” alisema mkazi huyo.
Pia wananchi hao walimtaka Waziri Shamsi Vuai Nahodha aondolewe madarakani kwa kushindwa kuulinda mkoa huo pamoja na kutowawajibisha wanajeshi waliokiuka maadili ya kazi zao wakati wakilinda usalama mara baada ya kutokea kwa vurugu.
Mwananchi mwingine alitaka Waziri Muhongo aondolewe kwa kuwa ameshindwa kusimamia suala hilo la gesi lililo chini ya wizara yake na hivyo kusababisa vifo, majeruhi na uharibifu wa mali.

Jumapili, 2 Juni 2013

Anna Kilango na Sophia Simba nusura Wachapane Hadharani


UHASAMA wa kisiasa kati ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na watoto, Sophia Simba na Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango, umevuka mipaka na sasa ni uadui wa wazi wazi. Hali hiyo ilidhihirika wiki iliyopita mjini Dodoma, wakati wawili hao walipokutana katika Benki ya CRDB iliyopo bungeni na badala ya kusalimiana, waliishia kutofautiana.
Shuhuda wa tukio hilo, aliiambia MTANZANIA, kuwa tukio hilo lilitokea saa 6 mchana, baada ya Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, kuahirisha Bunge kutokana na vurugu zilizosababishwa na wabunge wa upinzani, wakati wa mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Shuhuda huyo alisema kuwa, kabla ya tukio hilo, Anne Kilango pamoja na wabunge wengine wa CCM, walikuwa ndani ya benki hiyo wakibadilishana mawazo.

Wakati wakiendelea kuzungumza, Sophia Simba aliingia ndani na kuanza kuwasalimia kila mmoja kama ilivyo kawaida.

“Sisi tulikuwa hapa ndani ya benki pamoja na Diana Chilolo (Mbunge wa Viti Maalum CCM), Turky, Mbunge wa Mpendae (Salim Abdallah Turky) pamoja na wahudumu wa benki.

“Sofia Simba alipofika, alitusalimia lakini Anne Kilango hakuitikia salamu yake na hapo Sofia akasema, mheshimiwa Anne Kilango nakusalimia.

“Aliposema hivyo tu, Anne Kilango akahamaki na kusema usinisalimie, mimi sitaki salamu yako. Kauli hiyo ilionekana kutushangaza na wakati tunashangaa, Sofia Simba akasema, mheshimiwa Anne Kilango mimi ni shoga yako na tumetoka mbali, kwa nini tusisalimiane?

“Aliposema hivyo, Anne Kilango akasema sitaki kusikia salamu yako, ‘shut up’ kisha akaondoka,” alisema shuhuda huyo akinukuu maneno ya Anne Kilango.

Alipotakiwa kuzungumzia suala hilo kwa njia ya simu, Simba alisema kwa kifupi, kwamba, “nina ngozi ngumu, sizungumzi mambo haya kwa sababu mimi ni kiongozi,” alisema na kukata simu.

Naye, Anne Kilango alipoulizwa naye alisema yeye hawezi kuzungumzia masuala hayo, kisha akakata simu.

Mgeja ataka Sitta afukuzwe CCM kwa usaliti


SIKU chache baada ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, kutangaza timu inayoundwa na kundi lake kuwania urais 2015, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, amesema chama hicho kinatakiwa kumchukulia hatua za kinidhamu kwa sababu anahatarisha uhai wa chama.

Alisema, kama chama kitamuacha aendelee kutoa kauli zinazohatarisha uhai wa chama, CCM itajiweka katika mazingira mabaya kisiasa pindi wapinzani watakapoanza kuchambua kauli hizo.

Kauli hiyo ya Mgeja, aliyoitoa jijini Dar es Salaam jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari, imekuja ikiwa ni siku chache tu tangu Sitta aitaje timu inayoundwa na kundi lake kuwania ukuu wa dola mwaka 2015.

Alisema wanaounda timu hiyo ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe na Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, ambaye hata hivyo amekana kuwamo kwenye timu hiyo.

Jana akimzungumzia Sitta, Mwenyekiti huyo wa CCM, Mgeja alimshushia tuhuma nyingi akimwita mkorofi, mlalamishi na kwamba anaonekana wazi kukihujumu chama.

Mgeja pamoja na mambo mengine, alimshutumu Sitta kuwa alianzisha CCJ akiwa ndani ya CCM, kisha akataka kuhamia Chadema akiwa ndani ya CCM na yote hayo chama kiliyajua na kumwacha.

Alisema Sitta yeye ni waziri, lakini kuna wakati alikaririwa akisema kwamba, Serikali iwaombe radhi wananchi kwa sababu ya mgawo wa umeme, baadaye akasema maisha bora kwa kila Mtanzania hayawezekani na sasa amekaririwa hivi karibuni akisema Rais Kikwete alimhujumu kwenye uspika.

“Yaani anajiamini kiasi cha kuanza kumchokonoa hata Rais Kikwete, wakati akijua kwamba mambo anayoyafanya yanakwenda kinyume na mtazamo wa chama.

“Hivi huyu ni mtu gani asiyetosheka, kila wakati analalamika wakati yeye ni waziri na ana nafasi kubwa ya kupeleka malalamiko yake kwenye chama ili yakafanyiwe kazi.”

Alisema kama Sitta anaona yuko kwenye basi lenye abiria asioendana basi aondoke na kuhoji anafanya nini ndani ya CCM wakati anaonekana wazi kwamba haridhishwi na mwenendo wa chama na Serikali.

Mgeja pia alimtaka Sitta kwenda TAKUKURU kama anaona kuna rushwa ndani ya chama, au kama kuna wezi aende polisi na kama anaona kuna wahalifu, basi aende mahakamani.

“Lakini huyu mzee lazima chama kimchukulie hatua, huyu ni mzigo, kama hatadhibitiwa atakiharibu chama kwa sababu anaonekana ana ajenda ya siri,” alisema.

Mgeja aliitaka Kamati ya Maadili ya chama inayoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Philip Mangula, imjadili ili ijulikane ana ajenda gani.

Alisema kwa upande wake katika kikao cha NEC kijacho, atawasilisha hoja binafsi kutaka Sitta ajadiliwe.

“Yeye anajifanya ni msafi wakati mambo yake mengi tunayo, kwani hata alipopata uspika anaouota hadi sasa, alibebwa, tena kwa kampeni kali kweli kweli. Hivi, kwa nini asiwe kama mzee Msekwa (Pius Msekwa) ambaye baada ya kushindwa uspika alinyamaza kimya?” alifoka Mgeja.

Kwa mujibu wa Mgeja, kitendo kinachofanywa na Sitta ni cha hatari kwa uhai wa chama na kwamba kama isingekuwa huruma ya Mwenyekiti wa CCM, Taifa, Rais Jakaya Kikwete, angeshafukuzwa uanachama wa CCM.

“Kuna wakati tulikaa tukataka kumnyang’anya kadi na aliokolewa na Mwenyekiti wetu, lakini pamoja na kusamehewa, bado hatulii, anaendeleza mambo yake ya ajabu ajabu,” alisema.

Akizungumzia kauli ya Sitta ya wiki hii aliyoitoa akiwataja Magufuli, Membe na Dk. Mwakyembe kwamba ni wasafi, alisema ni ya kibaguzi, kwa kuwa waliotajwa ni Wakristo, wala hakuna Muislamu hata mmoja.

“Aliowataja wote hao akiwa kanisani ni wakristo, wala hakuna Muislamu, wote hao ni wanaume na hakuna mwanamke, pia hao wote ni kutoka Tanzania Bara na inavyoonekana Unguja na Pemba hakuna watu safi.

“Sasa mtu kama anadiriki kusema uongo, tena madhabahuni, ana sifa gani ya kuwa kiongozi, yaani amefika mahali sasa anaanza ubaguzi wa Watanzania Bara na Visiwani, anaanza kubagua jinsia, huyu hafai na lazima achukuliwe hatua.

“Namtaka anyamaze, asiendelee na mambo yake kwa sababu kama ataendelea kupiga porojo, nitasema mengi zaidi yanayomhusu kwa sababu siyo msafi kama anavyotaka kuwadanganya Watanzania,” alisema.

Alhamisi, 30 Mei 2013

Lipumba arekodiwa kwenye video 'akihamasisha UDINI' msikitini


Mwishoni mwa wiki zilipatikana taarifa za kushitua kumhusu Mwenyekiti wa Taifa cha Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba. Gazeti moja liliripoti kuwa limenasa mkanda wa video unaomwonyesha Prof. Lipumba si tu akikiri kuwa alimsaidia Rais Jakaya Kikwete kupata ushindi kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita bali pia ‘akihamasisha udini’ kwa kutaka Waislamu wajipange kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu ujao.
Awali nilitarajia mambo mawili, kwanza, Profesa Lipumba kupata ujasiri wa kufafanua kuhusu video hiyo, na pili, taarifa kutoka Ikulu aidha kukanusha au kufafanua kuhusu ‘msaada wa Prof Lipumba kwa Rais Kikwete.’ Hadi ninapoandika makala hii, hayo yote hayajatokea, na hivyo kilichozungumzwa na Lipumba kinaendelea kubaki halali.
Ni vema tutakumbuka kuwa hivi majuzi tu, Rais Kikwete alieleza bayana kuwa kuibuka kwa tatizo la udini kuna ‘mkono wa nchi za nje.’ Binafsi, nilitafsiri kauli hiyo ya Rais kama ‘kutoa majibu mepesi kwenye maswali magumu.’ Ninapata taabu kuamini maelezo ya Rais wangu kuhusu uhusika wa mataifa ya nje kwenye tatizo la udini hususan kwa sababu hakutaja japo nchi moja inayochochea tatizo hilo huko nyumbani.
Na kwa upande mwingine, kutaja tu uhusika wa mataifa ya nje hakutoi maelezo ya kutosha kwani bado kuna swali la; je, ni sera ya taifa fulani dhidi yetu au ni vitendo vya watu binafsi walio nje ya nchi dhidi ya taifa letu.’
Ukisikiliza kwa makini maelezo ya Prof Lipumba, unaweza kuelewa vyema jinsi udini ulivyotumika katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 ambapo Kikwete aliibuka mshindi. Lipumba amebainisha wazi kwenye video hiyo kuwa Waislamu walihamasishwa kumpigia kura Kikwete kwa matarajio kwamba angesaidia kutatua matatizo yao. Hata hivyo, kwa mujibu wa video hiyo, inaelekea kuwa matarajio hayo hayajatimia, na Lipumba amesikika akihamasisha Waislamu “Wajipange kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2015...kwa vile wenzetu (ninaamini akimaanisha Wakristo) wameshaanza kujipanga.”
Katika namna isiyopendeza kabisa, Prof Lipumba amejaribu kuifanya ajenda ya utajiri wa rasilimali tulionao, ambao unahujumiwa na mafisadi, kuwa ina uhusiano na ‘wenzetu’ (yaani Wakristo).
Nilitarajia Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, angekuwa mtu wa kwanza kutoa wito kwa Lipumba kuachia ngazi mara moja, kama ambavyo amekuwa ‘mwiba mkali’ kwa CHADEMA kiasi cha kujengeka picha kuwa Msajili huyo ni mithili ya mtumishi wa CCM.
Pamoja na ‘kumhukumu’ Prof. Lipumba kwa kauli zake, binafsi ninaamini kuwa alizungumza hayo si kama Mwenyekiti wa CUF bali muumini tu wa kawaida wa dini ya Kiislamu. Tatizo ni kwamba ni vigumu kutofautisha matamshi ya Lipumba mwanasiasa na Lipumba muumini. Lakini kibaya zaidi, bila kujali matamshi hayo yalitolewa na Lipumba katika wadhifa gani, madhara yake yanabaki kuwa makubwa.
Hivi tukiweka kando mkanda huo mmoja wa video, Prof Lipumba ameshapita katika misikiti mingapi akimwaga sumu hiyo ya udini? Je, Lipumba anaweza kuwathibitishia Watanzania kuwa kuna chama kimoja (ambapo ni dhahiri alimaanisha CHADEMA) kinafanya harakati za kuingia Ikulu kwa kusaidia na mataifa yasiyoutakia mema Uislamu?
Wakati hoja za mwanasiasa huyo msomi kuhusu jinsi nchi yetu ilivyo tajiri wa rasilimali lakini inakwamishwa na ufisadi unaolelewa na CCM zina mashiko, ‘tiba’ anayopendekeza ya kutumia udini si tiba bali ni sumu kali kabisa.
Ningependa kuchambua kwa undani zaidi kuhusu suala hili lakini nafasi hainiruhusu. Hata hivyo, ninaomba kuhitimisha makala hii kwa kutoa wito wa haraka kuwa Profesa Lipumba anastahili kujiuzulu mara moja.
Kauli zake za kuchochea udini hazina nafasi hata kidogo katika siasa za Tanzania hasa ikizingatiwa kuwa tatizo la udini limeshasababisha madhara kadhaa hadi sasa.
Kwa Lipumba kuendelea kubaki madarakani itarejesha picha ile ile ya mwaka 1995 kwamba CUF inatumia Uislamu kama silaha yake ya kisiasa, kwani haiwezekani chama kuwa chini ya Mwenyekiti anayehubiri udini pasipo chama hicho kuridhia udini kuwa ni moja ya sera zake.
Iwapo Lipumba atagoma kujiuzulu, basi ninaisihi CHADEMA (ambayo japo haikutajwa bayana kwenye video hiyo) ianzishe jitihada za kuhakikisha mwanasiasa huyo ‘anakwenda na maji.’
Kadhalika, ninataraji Msajili wa Vyama vya Siasa, Tendwa atatumia nguvu ile ile anayotumia dhidi ya CHADEMA kuchukua hatua stahili dhidi ya Prof Lipumba.
Vilevile, iwapo Lipumba hatojiuzulu, ninashauri waumini wa dini ya Kikristo kumshinikiza Lipumba ajiuzulu kwa sababu kamwe hatuwezi kuruhusu kuwepo kwa Uchaguzi Mkuu ambao mmoja wa wagombea urais (labda Lipumba atagombea tena mwaka 2015) ni mdini (angalau kwa mtizamo wake).
Nihitimishe makala hii kwa kutoa wito wa moja kwa moja kwa Profesa Lipumba kuwa licha ya kuthamini mchango wake kwa taifa na kimataifa, hususan katika nyanja za siasa na uchumi, alichokizungumza hakikubaliki hata kidogo. Na ni matarajio yangu kuwa atakuwa muungwana kwa sio tu kuomba radhi Watanzania pasi kujali itikadi zao za kisiasa na kidini, bali pia kujiuzulu uenyekiti wa CUF mara moja.
 Kwa wale wanaotaka kuangalia video angalia link hii http://www.chahali.com/2013/05/lipumba-arekodiwa-kwenye-video.html

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More