Akilitz Technologies

Ni wataalama walio bobea katika Teknologia ya habari na mawasiliano ya Kompyuta na mitandao ya inteneti

Ijumaa, 30 Agosti 2013

MWANAJESHI WA UN AUAWA NCHINI DRC

Umoja wa Mataifa umesema kuwa mwanajeshi wake mmoja wa kutunza amani ameuawa na wengine watatu kujeruhiwa kufuatia mapigano makali kati ya na wapiganaji wa waasi Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Msemaji wa Umoja wa Mataifa mjini New York, Farhan Haq, hata hivyo hajatangaza uraia wa wanajeshi waliouawa au kujeruhiwa. Wanajeshi hao wa Umoja wa Mataifa walitumia ndege za helicopta kuwasukuma nyuma wapiganaji wa M23 karibu na mji wa Goma, ambao ndio mji...

UINGEREZA INAWEZA KUISHAMBULIA SYRIA BILA IDHINA YA UN

Uingereza huenda ikaanzisha mashambulio dhidi ya utawala wa Syria, bila kuungwa mkono na Umoja wa Mataifa. Hayo ni kwa mujibu wa ushauri wa wataalamu wake wa masuala ya kisheria. Ushauri huo unasema, mashambulio hayo yatahitajika ikiwa yatatekelezwa ili kuzuia raia kuuawa, hata ikiwa wanachama wa kudumu wa baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Urussi na Uchina zikitumia kura zao za turufu kupinga mikakati za kijeshi dhidi ya utawala wa Syria. Maafisa...

Alhamisi, 22 Agosti 2013

Star wa "Prison Break" Wentworth Miller (MichaelScolfield) amejiweka wazi kuwa yeye ni Shoga

  Star wa "Prison Break",  Wentworth Miller  a.k.a Michael Scofield, amejitangaza kuwa yeye ni "Gay" (shoga), katika barua ya wazi aliyoiandika kwenda kwa Directoe wa St. Petersburg International Film Festival (tamasha la filamu la kimataifa la St. Petersburg) Muigizaji huyo (41) ameandika barua hiyo kukataa mualiko uliokuwa ukimtaka kuhudhuria tamasha hilo linalofanyika nchini kwao Russia na kwa mara ya kwanza kupitia barua hiyo amejitangaza kuwa yeye ni "Gay"...

Alhamisi, 8 Agosti 2013

Bilionea Wama dini Mererani auawa kwa risasi 20 Moshi

Moshi. Mfanyabiashara tajiri wa Mirerani na Jijini Arusha, Erasto Msuya, ameuawa kwa kupigwa risasi zaidi ya 20 kwa kutumia bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG), jana mchana. Erasto anayemiliki vitega uchumi kadhaa na anayeaminika kuwa miongoni mwa wafanyabiashara wa Mirerani wanaoongoza kwa utajiri, aliuawa jana saa 7:00 mchana wilayani Hai mkoani Kilimanjaro. “Eneo la tukio kumeokotwa maganda karibu 21 ya risasi zinazoaminika ni za SMG, yaani mwili ni matobo kila sehemu kwa kweli...

Ijumaa, 2 Agosti 2013

SAYANSI YA UFUFUAJI: MIAKA 20 IJAYO MADAKTARI WATAKUWA NA UWEZO WA KUWARUDISHIA UHAI WAGONJWA WALIOKATA ROHO!

Twende taratibu, hii ni taarifa ya kisayansi na sio ‘kiimani’ na imetolewa na daktari bingwa wa moyo wa Marekani. Sasa naomba uniruhusu nikuelezee nilichokutana nacho kuhusiana na habari hii. Dr Sam Parnia wa Marekani amedai kwamba kwa kupitia mbinu za kisasa za kitaalamu (kisayansi) kuna uwezekano wa kumrudishia uhai mgonjwa aliyekata roho ndani ya saa 24!! (hata mimi nimeguna) Dr ...

Jumatatu, 15 Julai 2013

CCM Chali, Chadema yaibuka kidedea Arusha

Chadema kimethibitisha umwamba wake katika siasa za Jimbo la Arusha Mjini, baada ya kutetea kwa kishindo kata zake nne kwenye uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika jana. Katika uchaguzi huo uliokuwa unasubiriwa kwa hamu na ambao ulichukuliwa kama kipimo cha siasa za Arusha ambazo zimekuwa na mvutano mkubwa, Chadema kiliongoza katikia vituo vyote 136 vya kupigia kura Kata za Elerai, Kaloleni, Kimandolu na Themi. Kata hizo zilikuwa wazi tangu mwaka 2011 baada ya Chadema kuwatimua wanachama...

Jumatatu, 1 Julai 2013

Rais Barack Obama awasili Tanzania

Rais wa Marekani Barack Obama, amewasili nchini Tanzania katika mkondo wake wa mwisho wa ziara yake barani Afrika. Ziara ya Obama inasemekana kulenga kuimarisha uhusiano wa kibiashara na Afrika huku kukiwa na wasiwasi kuwa Marekani inaachwa nyuma na China katika uhusiano wao na Afrika.  Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete na familia yake pamoja na maafisa wake wa serikali na wacheza densi za kitamaduni walimkaribisha Obama na familia yake mjini Dar es Salaam. Obama amewasili Tanzania baada...

Jumatatu, 24 Juni 2013

Brazil yazidi kusonga mbele Kombe la Mabara

Mshambuliaji wa Italia, Mario Balotelli (kushoto) akizuiwa na beki wa Brazil, David Luiz wakati wa mechi ya Mabara kwenye Uwanja wa Fonte Nova mjini Salvador. Picha AFP.   Brazil. Timu ya taifa ya Brazil juzi imeichapa Italia 4-2 katika mashindano ya Kombe la Mabara na hivyo Brazil kumaliza hatua ya makundi ikiongoza kundi A. Mshambuliaji Neymar wa Brazil katika mechi hiyo alifunga bao na hivyo kufikisha mabao...

Jumapili, 23 Juni 2013

Vigogo wahaha - wahojiwa mabilioni ya Uswis

Dar es Salaam. Suala la baadhi ya Watanzania kuhifadhi mabilioni ya fedha nchini Uswisi limechukua sura mpya, baada ya tume maalumu kuwahoji vigogo 200 wakiwamo wabunge, wanasiasa na wafanyabiashara. Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa tume hiyo inayoongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema tayari imeshafanya kazi hiyo kwa miezi miwili sasa. Tume hiyo maalumu iliyoundwa na Serikali kwa Azimio la Bunge lililotolewa mwishoni mwa mwaka jana, inatarajiwa kukamilisha...

Jumanne, 18 Juni 2013

Tizama matukio mbali mbali ya chama cha CHADEMA wakiwafariji wafiwa na majeruhi baada ya Mlipuko wa Bomu

Mwenyekiti wa Chadema, Mh Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema wakiwa nyumbani kwa wazazi wa mmoja wa marehemu (Ramadhani) eneo la Mianzini kuwapa pole kwa kuondokewa na mpendwa wao. Eneo la maafa. Inaelezwa kuwa wataalamu wa jeshi waligundua kuwako kwa kitu ndani yatanki la mafuta na hivyo kuamua kulikata. Taarifa hizo zinadai kwamba kulikuwa na mabomu yametegwa chini ya gari na hivyo tanki hilo lilishambuliwa kwa risasi labda utokee mlipuko! Pia gari hii ya matangazo...

Jumatano, 12 Juni 2013

TFDA: Kiwanda cha TPI kilisambaza ARV feki kwa Watanzania

MAMLAKA ya Chakula na Dawa (TFDA), imethibitisha dawa bandia za kupunguza makali ya Virusi Vya Ukimwi (ARV), zilitengenezwa na kiwanda cha Tanzania Pharmaceutical Industry (TPI). Taarifa hiyo, ilitolewa jana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Hiiti Sillo, wakati wa semina kwa wabunge iliyoandaliwa na Bohari ya Dawa (MSD). Sillo, alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali (NCCR-Mageuzi), aliyetaka kujua kama dawa hizo bandia za ARV kweli zilitengenezwa na kiwanda cha...

Messi na babake wadaiwa kulaghai serikali

Mshambulizi matata wa Barcelona Lionel Messi na babake wanachunguzwa nchini Uhispania kwa kuilaghai serikali ya nchi hiyo zaidi ya pauni milioni tatu nukta nne. Mchezaji huyo kutoka Argentina na babake, Jorge wanatuhumiwa kuibia serikali ya nchi hiyo, kwa kujaza fomu zizizokuwa za ukweli za marejesho ya kodi kati ya mwaka wa 2007 na 2009. Hata hivyo mechezaji huyo mwenye umri wa miaka ishirini na mitano hajasema lolote kuhusiana na madai hayo. Messi hulipwa Euro milioni kumi na sita...

Alhamisi, 6 Juni 2013

MTOTO WA MICHAEL JACKSON ATAKA KUJIUA

Imeripotiwa kuwa mtoto wa marehemu Michael jackson,Paris Jackson  amekimbizwa hospitalin baada ya kufanya jaribio la kujiuwa. Jackson Paris  mwenye umri wa miaka 15 sasa,alikimbizwa hospitali mapema Jumatano asubuhi na vyanzo kutuambia ilikuwa jaribio kujiua.Ripoti inasema kuwa alijiovadozi kwa dawa ambazo bado hazijafahamika Ndugu wa karibu na Paris jackson  wameuambia mtandao wa TMZ toka America kuwa hiyo yawezakuwa si jaribio la kwanza  kwani ana alama za  kujichanja...

BREAKING NEWS: MUME WA KHADIJA KOPA AFARIKI DUNIA

                              Khadija Omar Kopa akiwa na mumewe Jaffari Ally enzi za uhai wake Mume wa Malkia wa Mipasho Afrika Mashariki, Khadija Omar Kopa, aitwaye Jaffari Ally amefariki dunia usiku wa kuamkia leo. Marehemu alikuwa anasumbuliwa na matatizo katika mfumo wa upumuaji na mpaka mauti yanamfika alikuwa amelazwa katika hospitali ya...

Jumanne, 4 Juni 2013

KIBANDA AREJEA KUTOKA AFRIKA KUSINI, KWA KISHINDO

                                  Kibanda akiongea na waandishi wa habari alipowasili air port                                        Hapa...

Tizama picha zinazoonyesha kuwasili kwa mwili wa Albert Mangwea

Wasanii,waandaji,mashabiki na wadau wa muziki wa kizazi kipya Tanzania wameungana kupokea mwili wa marehemu Albert Mangwear pale Air Port Mchana wa leo.Albrt Mangweha "Ngwair" alifariki Jumanne iliyopita 28/5/2013 huko Afrika Kusini   Mwili wa marehemu Albert Mangweha a.k.a Ngawair ukiwa unapakiwa kupelekwa Airport kwa ajili ya kuletwa Tanzania....

Jumatatu, 3 Juni 2013

Maandamano yakutaka kumngoa JK yanaandaliwa

MAANDAMANO makubwa ya kutaka Rais Jakaya Kikwete asikilize kilio cha wakazi wa Mtwara na Lindi wanaopinga ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam yanaandaliwa. Baadhi ya wakazi wa Lindi na Mtwara kwa kushirikiana na Chama cha Wananchi (CUF), Juni 29 mwaka huu wanatarajia kufanya maandamano hayo kutoka makao makuu ya CUF Buguruni hadi Ikulu, jijini Dar es Salaam. Maandamano hayo pia yatakuwa na lengo la kumtaka Rais Kikwete awang’oe madarakani mawaziri watatu ambao ni Profesa...

Jumapili, 2 Juni 2013

Anna Kilango na Sophia Simba nusura Wachapane Hadharani

UHASAMA wa kisiasa kati ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na watoto, Sophia Simba na Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango, umevuka mipaka na sasa ni uadui wa wazi wazi. Hali hiyo ilidhihirika wiki iliyopita mjini Dodoma, wakati wawili hao walipokutana katika Benki ya CRDB iliyopo bungeni na badala ya kusalimiana, waliishia kutofautiana.Shuhuda wa tukio hilo, aliiambia MTANZANIA, kuwa tukio hilo lilitokea saa 6 mchana, baada ya Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, kuahirisha Bunge kutokana...

Mgeja ataka Sitta afukuzwe CCM kwa usaliti

SIKU chache baada ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, kutangaza timu inayoundwa na kundi lake kuwania urais 2015, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, amesema chama hicho kinatakiwa kumchukulia hatua za kinidhamu kwa sababu anahatarisha uhai wa chama. Alisema, kama chama kitamuacha aendelee kutoa kauli zinazohatarisha uhai wa chama, CCM itajiweka katika mazingira mabaya kisiasa pindi wapinzani watakapoanza kuchambua kauli hizo.Kauli...

Alhamisi, 30 Mei 2013

Lipumba arekodiwa kwenye video 'akihamasisha UDINI' msikitini

Mwishoni mwa wiki zilipatikana taarifa za kushitua kumhusu Mwenyekiti wa Taifa cha Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba. Gazeti moja liliripoti kuwa limenasa mkanda wa video unaomwonyesha Prof. Lipumba si tu akikiri kuwa alimsaidia Rais Jakaya Kikwete kupata ushindi kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita bali pia ‘akihamasisha udini’ kwa kutaka Waislamu wajipange kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu ujao. Awali nilitarajia mambo mawili, kwanza, Profesa Lipumba kupata ujasiri wa kufafanua...

Page 1 of 5812345Next

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More