Akilitz Technologies

Ni wataalama walio bobea katika Teknologia ya habari na mawasiliano ya Kompyuta na mitandao ya inteneti

This is default featured post 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Alhamisi, 30 Mei 2013

Lipumba arekodiwa kwenye video 'akihamasisha UDINI' msikitini


Mwishoni mwa wiki zilipatikana taarifa za kushitua kumhusu Mwenyekiti wa Taifa cha Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba. Gazeti moja liliripoti kuwa limenasa mkanda wa video unaomwonyesha Prof. Lipumba si tu akikiri kuwa alimsaidia Rais Jakaya Kikwete kupata ushindi kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita bali pia ‘akihamasisha udini’ kwa kutaka Waislamu wajipange kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu ujao.
Awali nilitarajia mambo mawili, kwanza, Profesa Lipumba kupata ujasiri wa kufafanua kuhusu video hiyo, na pili, taarifa kutoka Ikulu aidha kukanusha au kufafanua kuhusu ‘msaada wa Prof Lipumba kwa Rais Kikwete.’ Hadi ninapoandika makala hii, hayo yote hayajatokea, na hivyo kilichozungumzwa na Lipumba kinaendelea kubaki halali.
Ni vema tutakumbuka kuwa hivi majuzi tu, Rais Kikwete alieleza bayana kuwa kuibuka kwa tatizo la udini kuna ‘mkono wa nchi za nje.’ Binafsi, nilitafsiri kauli hiyo ya Rais kama ‘kutoa majibu mepesi kwenye maswali magumu.’ Ninapata taabu kuamini maelezo ya Rais wangu kuhusu uhusika wa mataifa ya nje kwenye tatizo la udini hususan kwa sababu hakutaja japo nchi moja inayochochea tatizo hilo huko nyumbani.
Na kwa upande mwingine, kutaja tu uhusika wa mataifa ya nje hakutoi maelezo ya kutosha kwani bado kuna swali la; je, ni sera ya taifa fulani dhidi yetu au ni vitendo vya watu binafsi walio nje ya nchi dhidi ya taifa letu.’
Ukisikiliza kwa makini maelezo ya Prof Lipumba, unaweza kuelewa vyema jinsi udini ulivyotumika katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 ambapo Kikwete aliibuka mshindi. Lipumba amebainisha wazi kwenye video hiyo kuwa Waislamu walihamasishwa kumpigia kura Kikwete kwa matarajio kwamba angesaidia kutatua matatizo yao. Hata hivyo, kwa mujibu wa video hiyo, inaelekea kuwa matarajio hayo hayajatimia, na Lipumba amesikika akihamasisha Waislamu “Wajipange kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2015...kwa vile wenzetu (ninaamini akimaanisha Wakristo) wameshaanza kujipanga.”
Katika namna isiyopendeza kabisa, Prof Lipumba amejaribu kuifanya ajenda ya utajiri wa rasilimali tulionao, ambao unahujumiwa na mafisadi, kuwa ina uhusiano na ‘wenzetu’ (yaani Wakristo).
Nilitarajia Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, angekuwa mtu wa kwanza kutoa wito kwa Lipumba kuachia ngazi mara moja, kama ambavyo amekuwa ‘mwiba mkali’ kwa CHADEMA kiasi cha kujengeka picha kuwa Msajili huyo ni mithili ya mtumishi wa CCM.
Pamoja na ‘kumhukumu’ Prof. Lipumba kwa kauli zake, binafsi ninaamini kuwa alizungumza hayo si kama Mwenyekiti wa CUF bali muumini tu wa kawaida wa dini ya Kiislamu. Tatizo ni kwamba ni vigumu kutofautisha matamshi ya Lipumba mwanasiasa na Lipumba muumini. Lakini kibaya zaidi, bila kujali matamshi hayo yalitolewa na Lipumba katika wadhifa gani, madhara yake yanabaki kuwa makubwa.
Hivi tukiweka kando mkanda huo mmoja wa video, Prof Lipumba ameshapita katika misikiti mingapi akimwaga sumu hiyo ya udini? Je, Lipumba anaweza kuwathibitishia Watanzania kuwa kuna chama kimoja (ambapo ni dhahiri alimaanisha CHADEMA) kinafanya harakati za kuingia Ikulu kwa kusaidia na mataifa yasiyoutakia mema Uislamu?
Wakati hoja za mwanasiasa huyo msomi kuhusu jinsi nchi yetu ilivyo tajiri wa rasilimali lakini inakwamishwa na ufisadi unaolelewa na CCM zina mashiko, ‘tiba’ anayopendekeza ya kutumia udini si tiba bali ni sumu kali kabisa.
Ningependa kuchambua kwa undani zaidi kuhusu suala hili lakini nafasi hainiruhusu. Hata hivyo, ninaomba kuhitimisha makala hii kwa kutoa wito wa haraka kuwa Profesa Lipumba anastahili kujiuzulu mara moja.
Kauli zake za kuchochea udini hazina nafasi hata kidogo katika siasa za Tanzania hasa ikizingatiwa kuwa tatizo la udini limeshasababisha madhara kadhaa hadi sasa.
Kwa Lipumba kuendelea kubaki madarakani itarejesha picha ile ile ya mwaka 1995 kwamba CUF inatumia Uislamu kama silaha yake ya kisiasa, kwani haiwezekani chama kuwa chini ya Mwenyekiti anayehubiri udini pasipo chama hicho kuridhia udini kuwa ni moja ya sera zake.
Iwapo Lipumba atagoma kujiuzulu, basi ninaisihi CHADEMA (ambayo japo haikutajwa bayana kwenye video hiyo) ianzishe jitihada za kuhakikisha mwanasiasa huyo ‘anakwenda na maji.’
Kadhalika, ninataraji Msajili wa Vyama vya Siasa, Tendwa atatumia nguvu ile ile anayotumia dhidi ya CHADEMA kuchukua hatua stahili dhidi ya Prof Lipumba.
Vilevile, iwapo Lipumba hatojiuzulu, ninashauri waumini wa dini ya Kikristo kumshinikiza Lipumba ajiuzulu kwa sababu kamwe hatuwezi kuruhusu kuwepo kwa Uchaguzi Mkuu ambao mmoja wa wagombea urais (labda Lipumba atagombea tena mwaka 2015) ni mdini (angalau kwa mtizamo wake).
Nihitimishe makala hii kwa kutoa wito wa moja kwa moja kwa Profesa Lipumba kuwa licha ya kuthamini mchango wake kwa taifa na kimataifa, hususan katika nyanja za siasa na uchumi, alichokizungumza hakikubaliki hata kidogo. Na ni matarajio yangu kuwa atakuwa muungwana kwa sio tu kuomba radhi Watanzania pasi kujali itikadi zao za kisiasa na kidini, bali pia kujiuzulu uenyekiti wa CUF mara moja.
 Kwa wale wanaotaka kuangalia video angalia link hii http://www.chahali.com/2013/05/lipumba-arekodiwa-kwenye-video.html

Ushoga walivunja Bunge


NAIBU Spika wa Bunge, Job Ndugai, jana alilazimika kuliahirisha Bunge mara mbili na kusitisha mjadala wa hotuba ya bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa baada ya wabunge wa CUF kumchachamalia mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje (CHADEMA).
Hatua hiyo ilikuja wakati Wenje akiwasilisha hotuba ya kambi ya upinzani na kutaja vyama vya siasa vya nje rafiki vinavyoshirikiana na vyama vya CCM, CHADEMA na CUF, akisema msimamo wa kiliberali wanaoufuata CUF unashabikia ushoga na usagaji.
Pamoja na Wenje kutokuwa ameufikia ukurasa wa nane uliokuwa na maneno hayo, hotuba yake ilikatizwa kwa mwongozo ulioombwa na mbunge wa Mtambile, Masoud Abdallah Salim (CUF).
Salim alitumia kanuni ya 68 (1) sambamba na 64 (1) (a) (c) akisema maneno yaliyotumika yanaudhi, kizandiki, kihuni, kishenzi, kifedhuri kisha akamtaka Wenje ayafute na kuwaomba radhi.
“Anasema kuwa chama cha CUF, kutokana na itikadi yake ya mrengo wa kiliberali ambayo miongoni mwa misingi yake mikuu ni pamoja na kupigania haki za ndoa ya jinsia moja, usagaji na ushoga.
“Kwamba hii ni kwa mujibu wa tangazo lao kwenye mtandao wao wa umoja wa maliberali ulimwenguni, likiungwa mkono na Waziri wa Haki na Usawa wa Uingereza, Lynn Featherstone, kutoka chama cha Liberal Democrats wakati chama hicho kilipokuwa kinapitisha azimio la kuruhusu ndoa za jinsia moja kama haki ya mtu mmoja mmoja,” alisema.
Salim aliitaka CHADEMA ifute maneno hayo na kisha kuomba radhi, vile vile Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge iwachukulie hatua, vinginevyo CUF walitishia kuchukua hatua.
Wakati Salim akiomba mwongonzo huo, wabunge wa CUF na CCM walikuwa wakichagiza kwa maneno ya chini kwa chini wakisema…wamezoea hao, wapigwe, waondoe maneno, washenzi…wakome kabisa.
Baada ya mbunge huyo kumaliza, Naibu Spika, Job Ndugai, alimuuliza Wenje kama ana lolote la kusema na ndipo akaomba wabunge wenzake wamsikilize na kujaribu kuelewa alikuwa akimaanisha nini.
“Kwa heshima kubwa naomba wabunge wanielewe, hapa tumeeleza vyama vya nje vyenye mahusiano na vyama vya hapa ndani, nilieleza CCM ilivyo na mahusiano na vyama vya kikomunisti, CHADEMA inahusiana na vyama vya kidemokrasia na CUF inahusiana na vyama vya kiliberali, hapa tunazungumzia itikadi,” alisema Wenje.
Hata hivyo, hotuba yake ilikatizwa na wabunge wa CUF waliokuwa wakiongozwa na Salim, wakisimama na kuanza kuporomosha maneno mazito wakisisitiza hotuba hiyo haisomwi, huku wengine wakichana vitabu vya hotuba hiyo.
Ndugai baada ya kuona hali hiyo, ambapo baadhi ya wabunge hao wakiwemo wa CCM walikuwa wakichochea wakitaka Wenje apigwe alitangaza kuliahirisha Bunge kwa muda hadi saa 11 jioni na kuomba Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ikutane.
Licha ya Bunge kuahirishwa, mzozo uliendelea ndani ya ukumbi wa Bunge kwa wabunge wa CUF kutaka kumpiga Wenje.
Wakati vurugu hizo zikiendelea wabunge wengi wa CHADEMA hawakuwemo ukumbini maana walikuwa kwenye kikao na mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kwenye ofisi za kambi, jambo lililowafanya askari wa Bunge kusogea karibu na Wenje.
Bunge laahirishwa tena
Baada ya mapumziko ya mchana Bunge lilianza kwa Ndugai kumwita Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maadili, John Chiligati, kueleza uamuzi uliofikiwa.
Chiligati alisema kuwa walikutana na Salim kama mlalamikaji ambaye msimamo wake ulikuwa ni kumtaka Wenje aombe radhi na kuondoa maneno hayo, masharti ambayo Wenje alikubaliana na moja la kuondoa maneno.
“Lakini aliiahidi kamati kuwa anakwenda kuibadili hotuba yake kwa kuondoa maneno hayo lakini hakuna mabadiliko aliyofanya maana maneno aliyoweka kwa Kingereza ni yaleyale aliyotakiwa kuondoa,” alisema.
Hata hivyo, Wenje alipopewa muda aseme kama anakubaliana na ushauri huo, alitoa ufafanuzi huku akionyesha nyaraka za makubaliano ya vyama vya kiliberali yaliyofikiwa mwaka 1997 na CUF kikiwa mshiriki, kisha akakataa kuomba radhi kwa maelezo kuwa haoni kosa.
Kutokana na msimamo huo, Ndugai alimwamuru Wenje kuomba radhi na kuondoa maneno hayo ndipo aweze kuendelea na hotuba yake, lakini mbunge huyo aligoma katakata kuomba radhi na hivyo akatakiwa kuketi.
“Suala hili nalirudisha kwenye kamati ya maadili ili itushauri zaidi na kwa hali hiyo siwezi kuendelea, nasitisha Bunge hadi kesho saa tatu asubuhi na tutaendelea na Wizara inayofuata ya Uvuvi na Maendeleo ya Mifugo,” alisema Ndugai.
Wabunge welionekana kubishana kwenye makundi nje ya ukumbi huku wengi wa CCM na CHADEMA wakimsifu Wenje na kumlaumu Ndugai kuwa alishindwa kulimudu Bunge.
Mapema asubuhi
Vugugu hizo zilihamia nje ya Bunge ambapo wabunge wa CUF walikuwa wakimfuata Wenje ili kumshambulia lakini wabunge wenzake wa CHADEMA na CCM walimsihi asifanye malumbano na hivyo kumsindikiza hadi ofisi za kambi hiyo wakiongozwa na Livingstone Lusinde.
Wabunge wa CUF walikuwa wakiporomosha maneno makali na matusi dhidi ya Wenje na viongozi wengine wa CHADEMA wakiapa kuwa liwalo na liwe lakini hotuba hiyo haitasomwa hadi maneno hayo yaondolewe.
Baadhi yao, Khatib Haji (Konde), Bungala (Kilwa Kusini), Ibrahim Sanya (Mji Mkongwe), Rukia Kimwaga (Viti Maalum), Salim (Mtambile) na wengineo walikuwa wakiporomosha matusi mazito wakidai kuwa CHADEMA inawadhalilisha wakati chama chao kimekuwa mstari wa mbele kupinga vitendo vya ushoga.
Hata hivyo, mabishano hayo yaliibua pande mbili ambapo baadhi ya wabunge wengi wa CCM walikuwa wakiwaunga mkono CUF wakati wengine walikuwa wakipinga na kusema kuwa hawakufasiri vyema maneno ya Wenje.
“Wacha iwapate maana wakati tulipolalamikia hotuba za CHADEMA kuwa na maneno ya kuudhi dhidi ya CCM walikaa kimya, sasa kwa nini nao wasingekuwa wavumilivu hadi amalize hotuba yake. Kwanza ukurasa wenyewe alikuwa hajaufikia pengine angeruka,” alisema mbunge wa CCM.
Naye Ndugai, aliwarushia lawama waandishi wa habari akidai kuwa wanaibeba CHADEMA hata pale wabunge wake wanapofanya mambo ya hovyo.
“Hawa wanakwenda kuwa watawala, sasa kwa mwendo huu unadhani itakuwaje lakini nyie waandishi ndio mnawabeba. Hizi hotuba tunajua sio za kambi wanaandika wenyewe,”
Hata hivyo Ndugai alikwepa kufafanua ni kwa nini kiti cha Spika hakizipitii mapema kabla ya kusomwa bungeni.

Jumanne, 28 Mei 2013

KILICHOMUUA MANGWEA HIKI HAPA.. BOFYA HAPA KUSOMA HABARI ZAIDI


HABARI za kusikitisha zilizopatikana jioni ya leo ni kwamba msanii wa muziki wa bongo fleva, albert Mangwair maarufu kam,a ;ngwair' amefariki dunia akiwa nchini Afrika kusini.
Imethibitika ni kweli Mangwea amefariki dunia leo.
Mangwair ambaye anadaiwa alikuwa huko kwa ajili ya shughuli za kimuziki, alifia kwenye hoteli moja baada ya kutoiamka tangu alipolala usiku wa jana.
Taarifa hizo zisizo rasmi zinaeleza kwamba, nyota huyo alizidisha kiwango cha dawa za kulevya ambacho ndio chanzo cha kifo chake.
Kifo cha ngwair ambaye alikuwa ni muasisi wa kundi la Chamber squad la jijini Dar es salaam, kimeleta simanzi kubwa kwa wadau wa muziki huo.
Ngwai ambaye alikuwa na kipaji cha pekee cha kuimba kwa mtindo huru 'free styles' alipata kutamba na nyimbo kama GHETO LANGU, HOSTEL, MIKASI, SPEED 120, TUPO JUU N.K.
msiba wa msanii huyo upo nyumbani kwa mama yake huko Kihonda njia ya kuelekea Mazimbu mjini Morogoro huku familia nayo ikigubikwa na utata juu ya taarifa za kifo hicho.
RIP

Sitta: Asema JK alinihujumu


WAZIRI wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amewatuhumu viongozi wenzake ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa walishiriki kwenye njama ovu za kumnyang’anya uspika kwa sababu waliogopa spidi na viwango vyake.
Sitta alitoa kauli hiyo jana wakati alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustine (SAUT), Mwanza.
Ingawa Sitta hakuwa tayari kutaja majina ya viongozi hao waliomhujumu, ni wazi kuwa tuhuma hizo zinamwelekea moja kwa moja Rais Jakaya Kikwete, ambaye ndiye aliongoza vikao vya kupitisha jina la mgombea uspika.
Inafahamika pia kuwa Rais Kikwete ndiye aliyeleta wazo la kuwa na spika mwanamke, kigezo ambacho Sitta asingeweza kukitimiza.
Awali kabla ya kufanyika kwa vikao hivyo mwaka 2010 kulikuwa na tetesi kuwa Sitta hatakiwi kurejea kwenye kiti hicho kwa sababu alichangia kushamiri kwa upinzani na migogoro ndani ya CCM.
Baadhi ya wagombea wa CCM waliojitokeza kuchuana na Sitta katika kuwania nafasi hiyo ni Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, na Anna Makinda. Itakumbukwa kuwa wakati anagombea uspika, Sitta alikuwa ndiye Spika kwa miaka mitano iliyotangulia (2005-2010).
Alisema hujuma hiyo ililenga kumstaafisha kwa lazima kabla ya muda wake, kwa kisingizio cha wakubwa zake hao kutaka Bunge liongozwe na mwanamke, jambo ambalo alionekana kutoridhishwa nalo.
“Siku zote mimi ni mtu wa viwango na ukweli. Hata wakati nilipokuwa Spika wa Bunge, baadhi ya wakubwa zangu wa kazi hawakufurahishwa na uwazi, viwango na spidi yangu ya kuongoza Bunge.
“Kwa sababu ya baadhi ya wakubwa wangu kutofurahishwa na viwango vyangu, nilistaafishwa Uspika kabla ya muda wangu. Sababu na kisingizio chao, eti huu ni wakati wa Bunge kuongozwa na mwanamke!. Hii mmh,” alisema.
Wajuzi wa siasa ndani ya CCM wanasema kwamba hii ilikuwa mara ya pili kwa Rais Kikwete “kumhujumu” Sitta. Mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2005 kwa kumnyima uwaziri mkuu ambao Kikwete alikuwa amemuahidi wakati wa mchakato ndani ya kundi lake la wanamtandao.
Katika mtandao huo, Kikwete alikuwa na watu wawili aliokuwa amewaahidi uwaziri mkuu – Sitta na Edward Lowassa – kila mmoja kwa muda wake. Hata hivyo, habari za ndani zinaeleza kuwa mara baada ya kushinda, Rais Kikwete alibadili msimamo, kwa kigezo kuwa alikuwa anapata wakati mgumu kumpa uwaziri mkuu mtu ambaye (yeye Kikwete) angemmwamkia “shikamoo.”
Huo ndio ulikuwa mwanzo wa njama za kumwondoa Spika aliyekuwapo, Pius Msekwa, na kumhamasisha Sitta agombee uspika. Kundi la wanamtandao lilimpiga vita Msekwa likimwita “agano la kale,” likahakikisha Sitta anapita.
Hata hivyo, Sitta alifanya kazi ya uspika kwa msuguano mkubwa kati yake na Waziri Mkuu wa wakati ule, Edward Lowassa, ambaye alijiuzulu mwaka 2008 kwa shinikizo la Tume ya Bunge kuhusu kashfa ya kampuni tata ya kufua umeme, Richmond.
Kuhusu ufisadi, Sitta alisema amejipambanua kupambana nao pasi na woga kwakuwa anaamini hiyo ndiyo nia nzuri ya kuliokoa taifa.
Aliongeza kuwa wapo baadhi ya watu hapa nchini wanafanya biashara ya unyonyaji na wanasafirisha fedha nje ya nchi.
Alisema biashara hizo za kiunyonyaji ndizo zinazosababisha mikopo ya elimu kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kuendelea kucheleweshwa, na aliwataka wasomi na Watanzania wote kutokukubali nchi kushikwa na mafisadi, kwani watu hao ni hatari na hawana huruma na uchumi wa taifa.
“Mpaka leo hii namsifu sana Baba wa Taifa, hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa uadilifu aliokuwa nao. Aliona mbali, alipiga vita ukabila na unyonyaji wa rasilimali za nchi. Hivyo, tusiruhusu tabaka la watu wanyonyaji kuongoza uchumi wa taifa hili,” alisema Sitta.
Alisema, yeye binafsi kamwe hakubaliani na vitendo vya kifisadi vinavyofanywa na baadhi ya watu, hivyo wasomi na Watanzania wasiunge mkono watu walioihujumu nchi kupitia mikataba mingi mibovu ya kifisadi.
Aidha, Waziri Sitta alieleza kusikitishwa na usiri wa mambo unaofanywa na Serikali kuhusu maendeleo ya nchi, na alitaka usiri huo usiwepo, huku akihoji: “Utaendeshaje nchi kwa usiri? Kwa nini ufanye siri kuhusu mambo ya kimaendeleo kwa wananchi wako?”
Aliponda pia kasi ndogo ya ukuaji wa uchumi wa nchi unaoonekana sasa kwa kukua kwa asilimia 6.9 kwa mwaka, badala ya kukua kwa asilimia 10 hadi 12 kwa mwaka, na aliwalaumu baadhi ya viongozi nchini kutazama suala la kuongeza ajira badala ya kupigania ukuaji wa uchumi wa taifa.
Kustaafu ubunge
Alisema hivi sasa anafikiria kustaafu ubunge, na tayari ameshawaambia wapiga kura wa Urambo Mashariki juu ya azima yake hiyo.
Alisema ni vema na viongozi wengine wakafikiria kustaafu siasa baada ya kuwatumikia wananchi kwa kipindi kirefu.
“Viongozi wenzangu msipende kung’ang’ania madaraka. Nawaombeni mjifunze kusema yatosha …staafuni kama ninavyotaka kufanya mimi,” alisema.
Jitihada za kupata wasaidizi wa Rais Kikwete kuzungumzia kauli ya Sitta hazikuzaa matunda, kwani simu zao katika kitengo cha mawasiliano Ikulu, zilikuwa zimezimwa hadi tunakwenda mitamboni.

Dk. Mwakyembe aundiwa zengwe bandarini


MAKUNDI mawili yenye nguvu kifedha na madaraka katika mamlaka za Serikali yanapanga njama ili kukwamisha jitihada za Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe. Makundi hayo yametajwa kutoka Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA) na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambao kwa pamoja wanadaiwa kuunganisha nguvu ili kupunguza kasi ya kuwafukuza watumishi wa bandari inayolenga kuziba mianya ya rushwa.
Baadhi ya watumishi TPA waliliambia MTANZANIA kuwa mkakati huo ulianza baada ya Dk. Mwakyembe kufanya operesheni ya kuwatimua baadhi ya watumishi wa bandari.

Walisema Dk. Mwakyembe amekuwa akifanya maamuzi mazito, ikiwemo kufukuza watumishi wa bandari na kuwasimamisha wengine.

“Si kazi rahisi kupata kazi bandari ukizingatia hali yenyewe ilivyo ya kupata ajira, kwanza unapata kazi kwa kuhonga hata kama una sifa zinazostahili,” walisema.

Mmoja wa wafanyakazi wa TPA, alisema Dk. Mwakyembe aliwahi kuagiza kurudishwa haraka scanner ya kupimia mizigo iliyoondolewa Bandari ya Dar es Salaam na kupelekwa Bandari ya Tanga, lakini hadi sasa haijarudishwa.

Alisema scanner hiyo ilipelekwa kwa kificho zaidi ya miaka mitatu iliyopita na haijawahi kufanya kazi yoyote huko mkoani Tanga.

Msemaji wa TPA, Janet Ruzangi alikiri scanner hiyo kupelekwa Tanga chini ya usimamizi wa TRA.

Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitilya hakupatikana kuzungumzia suala hilo, baada ya wasaidizi wake kutaka aandikiwe maswali.

Hata hivyo, licha ya maswali hayo kuandikwa, ni zaidi ya wiki mbili sasa hakuna majibu yaliyo

Source: Gazeti la Mtanzania

Jumatatu, 27 Mei 2013

Waliofeli kidato cha nne waula, ufaulu sasa waongezeka


Dar es Salaam. Idadi ya watahiniwa waliofaulu mtihani wa kidato cha nne mwaka jana imeongezeka kwa kati ya asilimia 20 na 23 baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), kufanya marekebisho alama za viwango vya ufaulu, Mwananchi limebaini.
Habari ambazo gazeti hili imezipata zinasema matokeo hayo ambayo yamewezesha kiwango cha ufaulu kupanda na kufikia asilimia kati ya 54 na 57, huenda yakatangazwa wiki hii pamoja na yale ya kidato cha sita ambayo pia yamechelewa kutangazwa.
Chanzo cha habari kutoka Necta kimesema matokeo hayo mapya yanaonyesha kuwa, ufaulu wa kuanzia daraja la kwanza hadi la nne umeongezeka kutoka asilimia 34.5 kwa matokeo yaliyotangazwa awali na huenda yakafikia asilimia 57. Hii inamaanisha kwamba watahiniwa wapatao 82,000 ambao awali walikuwa wamepata sifuri katika matokeo ya awali sasa wamepanda na kupata madaraja ya ufaulu katika matokeo mapya.
Kwa matokeo hayo, watahiniwa wa mwaka 2012 watakuwa wamefanya vizuri kuliko wa mwaka 2011, ambao watahiniwa 225,126 sawa na asilimia 53.37 ya 349,390 waliofanya mtihani huo walifaulu.
Msemaji wa Necta, John Nchimbi alisema upangaji wa matokeo hayo ulikuwa bado unaendelea. “Ninachojua kwa sasa ni kuwa mchakato unaendelea na matokeo yatatangazwa mapema tu ili watoto waweze kujiunga na shule mapema,” alisema Nchimbi.
Pia alisema usahihishaji wa mitihani ya kidato cha sita umekamilika.
Matokeo ya awali
Matokeo ya awali yaliyotangazwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa yalionyesha kuwa kati ya watahiniwa 367,756 waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana, waliokuwa wamefaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu walikuwa 126,847 sawa na asilimia 6.4. Waliopata daraja la nne walikuwa ni 103,327 sawa na asilimia 28.1.
Katika matokeo hayo, watahiniwa 240,909 sawa na asilimia 65.5 walipata sifuri, hesabu ambayo imebadilika katika matokeo mapya ambayo yanaonyesha kuwa sasa waliopata daraja hilo ni 158,100 ambayo ni asilimia 43.
Hata hivyo, habari kutoka Necta zinasema kuwa licha ya kuwezesha kuongezeka kwa waliofaulu, matumizi ya kanuni mpya ya kukokotoa matokeo hayo yalisababisha zaidi ya wanafunzi 2,500 kushuka ufaulu ikilinganishwa na awali.
Maofisa mbalimbali wa Necta pamoja na wale wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na taasisi zake, walikutana mwishoni mwa wiki iliyopita kukubaliana masuala mbalimbali juu ya matokeo hayo pamoja na suala la matokeo ya wanafunzi hao 2,500 kabla ya kutangazwa wiki hii.
“Baada ya wajumbe kujadili suala lile, busara ilibidi itumike kwa hiyo hakuna mwanafunzi ambaye alama yake itashuka, kwa kawaida isingewezekana mtoto ambaye matokeo yalitoka akiwa amefaulu leo umwambie ameshuka,” kilieleza chanzo chetu.

Chadema yaipunguza kasi CCM Tabora

*Viongozi CCM wazomewa katika mkutano wa hadhara
*Ni baada ya kuanza kuwatukana viongozi wa Chadema

Mbunge wa Tabora Mjini, Aden Rage













VIONGOZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Tabora, juzi walijikuta katika wakati mgumu, baada ya kuzomewa na wananchi kwenye mkutano wa hadhara. Tukio hilo la aina yake lilitokea wakati viongozi wa chama hicho ngazi ya mkoa, akiwemo Mbunge wa Tabora Mjini, Aden Rage, walipokwenda kuhutubia mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Stendi ya mabasi ya zamani mjini hapa.

Mkutano huo wa hadhara ulifanyika siku chache baada ya ule wa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe, ambaye aliwaeleza wananchi, kuwa wabunge wa CCM mkoani Tabora hawawakilishi vema wapigakura wao na kwamba kutokana na hali hiyo, wabunge wa Chadema wameamua kupigania haki zao.
Baada ya Zitto kuhutubia katika uwanja huo, viongozi wa CCM waliamua kujibu mapigo wakiongozwa na Rage ambapo juzi waliamua kuitisha mkutano huo.

Dalili za CCM kuzomewa katika mkutano huo, zilianza mapema kabla ya kuanza kwa mkutano kwani baadhi ya wananchi walisikika wakikejeli kwamba wanataka kusikia sera si majigambo, matusi wala blaa blaa nyingine.

“Tunataka barabara za lami kuanzia Tabora-Nzega, Tabora-Urambo na ile ya Itigi-Tabora, vinginevyo wapisheni peoples power,” walisikika baadhi ya wananchi wakisema.

Wakati hayo yakitokea, Katibu wa CCM, Mkoa wa Tabora, Idd Ame, alianza kuhutubia huku akikiponda Chadema jambo ambalo liliwakera wananchi na kuanza kumzomea.

“Ndugu zangu wananchi, hebu angalieni mnavyodanganywa, hivi hawa Chadema wanajigamba kujenga barabara wakati wao siyo watoaji wa fedha, Serikali ya CCM ndiyo yenye dhamana ya fedha wala siyo hao wanafiki na waongo wakubwa.

“Mtu anaacha jimbo lake huko Kigoma anakuja hapa Tabora kuwafundisha siasa chafu, huu ni ‘upumbavu’ hatuwezi kuuvumilia,” alisema Ame.

Baada ya kauli hiyo, mkutano ulivurugika na wananchi walianza kuzomea kwa maneno ya kejeli wakidai wanataka sera na siyo matusi, huku wengine wakisema CCM ni wepesi wa kujibu hoja za Chadema na siyo kuanzisha hoja zao wenyewe.

Aidha, katibu huyo aliendelea kuwaambia wananchi kuwa kama wataendelea na tabia ya kuwasikiliza Chadema, watasababisha mapigano bila kutarajia.

“Hapa tuko kamili, endeleeni kuzomea tu, tutaumizana kweli kweli, hapa msifikiri hatuwezi na tutawashitaki viongozi wa Chadema Tabora kwa kutufanyia fujo kwenye mkutano wetu,” alisikika akisema Ame.

Wakati akisema maneno hayo, yaliyoonekana kutowafurahisha baadhi ya viongozi wa meza kuu ambapo, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), John Mchele, aliamua kwenda kumnong’oneza katibu huyo ili aache malumbano na wananchi.

Huku mkutano huo ukikosa utulivu, fujo kubwa zilizuka baada ya vijana wa ulinzi wa CCM wanaojulikana kama ‘Green Guard’ kuamua kutuliza vurugu hizo.

Baada ya vurugu kutulia kidogo, Rage alipanda jukwaani kuhutubia na baadaye alitoa Sh milioni 68 kwa kata kumi za Manispaa ya Tabora, ambapo kila kata ilikabidhiwa hundi yake kwa ajili ya miradi ya ujenzi wa vyoo, umaliziaji nyumba za walimu pamoja na madarasa.

Pia, Rage alikabidhi pikipiki mbili kwa chama cha waendesha bodaboda na kuahidi kuendelea kutoa misaada mingine kadiri atakavyoweza.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa CCM Tabora Mjini, Moshi Nkonkota, alilitupia lawama Jeshi la Polisi, kuwa hawataki kulinda mikutano ya CCM na kusababisha wafanyiwe vurugu.

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More