Jumapili, 28 Aprili 2013

Arsenal yaibana Man United


Ligi kuu soka nchini Uingereza imeendelea kwa michezo mitatu iliyopigwa kwenye viwanja vitatu tofauti jijini London jumapili hii.

Manchester United ambao ni mabingwa wa ligi hiyo msimu huu, Hii leo walikuwa wageni wa Arsenal kwenye uwanja wa Emirates Kaskazini mwa london,
Theo Walcot alianza kuifungia Arsenal bao la mapema kabisa dakika ya pili ya mchezo huo ambao BBC ulimwengu wa soka ilikuwa ikuutangaza moja kwa moja.
United walio chini ya Sir Alex Ferguson walionekana kutokuwa kwenye kiwango chao kama mabingwa baada ya kuanza mchezo huo kwa kufanya makosa mengi, na kujikuta wakipewa kadi nne za njano ndani ya dakika 30 za mchezo huo.
Lakini makosa ya safu ya ulinzi wa Arsenal, hasa lile la beki Bakar Sagna la kurudisha mpira kwa kipa wake yaani back pass yaliifanya United isawazishe bao lao kwa njia ya penati baada ya Sagna kutaka kufuta makosa kwa kumchezea vibaya Robin Van Persie ambaye aliifunga timu yake ya zamani bila ya kushangilia.
Dakika 90 zilimalizika kwa timu hizo kugawana pointi na Arsenal kufikisha pointi 64 pointi mbili zaidi ya wapinzani wao Tottenham ambao walitoka sare pia hapo jana na Wigan.
Kwingineko Mashariki mwa jiji la London kulikuwa na michezo miwili kwenye viwanja tofauti,
Chelsea wakiwa wenyeji wa Swansea kwenye uwanja wa Stamford Bridge, Mchezo uliomalizika kwa vijana wa Roman Abromavich kuibuka na ushindi wa 2-0, Mabao yao yakifungwa na Mbrazil Oscar Dos Santos Junior huku Frank Lampard akifunga kwa mkwaju wa penati.
Na Mchezo wa awali kabisa ulichezwa kwenye uwanja wa Roftus Road kwa QPR kupambana na Wigan, Mchezo ambao ulimalizika kwa sare bila kufungana.
Matokeo hayo ya sare kwa QPR na Wigan yalizifanya timu zote mbili kushuka daraja la ligi kuu.
Mechi nyingine itapigwa hapo kesho kati ya Aston Villa na Sunderland, Mechi ambayo itakuwa ni ya kukata na shoka kwani timu zote mbili zinajitutumua kutoshuka daraja.
CHANZO: bbc.uk

0 maoni:

Chapisha Maoni

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More