Jumamosi, 13 Aprili 2013

Wenye nyumba mijini wanapogeuka miungu watu

TUMEUANZA mwaka mpya kwa mambo yale yale kama ilivyokuwa mwaka uliopita.
Akili za wengi zipo kwenye harakati za maendeleo, karo za watoto wao na ugumu wa maisha unaowakabili wengi.
Kingine ni kodi ya pango, mdudu ambaye hunyanyasa wengi hasa wa kipato ha chini.
Lakini, kila anayemiliki  nyumba katika maeneo ya mijini hasa hasa katika majiji kama Mwanza, Dar es Salaam, Arusha na Mbeya, hakika anaitwa mbarikiwa.
 Anaitwa mbarikiwa kwa sababu nyingi. Kwanza, ardhi ni kitu cha thamani, pili ujenzi ni gharama na anayefanikiwa…hakika huyo amejikwamua kiuchumi na kijamii.
Wamiliki wengi wa nyumba wapo katika makundi kadhaa, kuna wanaoishi katika nyumba zao bila kupangisha na wengine wanaozikodisha na kujipatia fedha.
 Dhamira nzima ya wino huu inadondokea kwa wale wanaopangisha nyumba zao  yaani…wenye nyumba.
Ama kwa hakika wenye nyumba wengi wamekuwa kama miungu watu. Baadhi yao wamejivika kilemba cha utukufu na kutumia rasilimali zao kwa unyanyasaji wa hali ya juu.
 Mara kadhaa unapokwenda kutafuta nyumba si ajabu ukapewa masharti ya ajabu. Kwa mfano, wapo wanaoambiwa wasipike aina fulani ya mboga, wasiwe na watoto au wakanyimwa kuleta wageni.
 Lakini, pia wapo wenye nyumba ambao wanataka wamtawale mpangaji kama mtoto wao kwa kumwekea masharti hata ya kutoka na kurudi saa ngapi.
 Haya yote yanasababishwa na sheria  butu za nyumba  nchini ambazo husababisha wenye nyumba kujigeuza miungu kwa sababu tu wanamiliki nyumba.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More