Jumanne, 30 Aprili 2013

Borussia Dortmund yapeta - Real Madrid 2-0 Borussia Dortmund


Borussia Dortmund imejikatia tiketi ya kuingia fainali ya Klabu bingwa Ulaya 2012-13 baada ya kupata ushindi wa jumla ya magoli 4-3 dhidi ya Real Madrid. Real Madrid imeshinda 2-0  katika mechi ya nusu fainali  ya pili katika Bernabeu Jumanne. Lakini imeshindwa kusonga mbele kutokana na kipigo ilichopata cha magoli 4-1 Kutoka kwa Borussia Dortmund walipokuwa nyumbani wiki iliyopita.
Upande wa timu hiyo ya Bundesliga ulinusurika kutolewa katika kinyang’anyiro hicho. Na kama Rael Madrid wangefanikiwa kuongeza goli moja wangekuwa pazuri zaidi kwakuwa na goli moja la ugenini. Lakini bahati haikuwa upande wao na hivyo kupoteza nafasi hiyo na kutolewa
Hata hivyo, magoli kutoka Karim Benzema na Sergio Ramos katika dakika 10 za mwisho  ghafla ilianzisha nguvu mpya, lakini Dortmund ikiwa juu kimagoli wameingia fainali ya kwanza tangu mwaka 1997, wakati ilipofungwa Juventus 3-1.
Vijana wa Mourinho walijua ukubwa wa kazi waliyokuwa nayo, na walianza mchezo kwa umakini wakiwa na kiu ya kufanya mapinduzi. Gonzalo Higuain angeweza kufungua mchezo kwa bao mnamo dakika nne, lakini shuti alilounganisha toka kwa Mesut Ozil liliishis mikononi mwa Weidenfeller Roman.
Lewandowski alikosa kutoka yadi nane, kabla ya Madrid hatimaye alionyesha dalili ya uhai katika nusu ya pili.
Benzema akitokea benchi wakati zikiwa zimesalia dakika saba, alionyesha uhai na kuipa timu yake nguvu ya kuusaka ushindi baada ya kuipatia goli timu hiyo ya hispania.
Madrid ilipata jumla ya magoli 2 katika mechi hiyo ingawa magoli hayo hayakutosha kuiwezesha timu hiyo kusonga mbele kwenye hatua ya fainali
Sasa swali kuu ni je Wembley zitacheza timu zote za kijerumani ama Barcelona inaweza kufanya mabadiliko hapo kesho?

0 maoni:

Chapisha Maoni

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More