Ijumaa, 12 Aprili 2013

Madudu Serikalini







RIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, imewasilishwa bungeni huku ikiendelea kueleza madudu mengi yaliyopo serikalini. Ripoti hiyo, inayoishia Juni 2012, iliwasilishwa jana kisha ikatolewa ufafanuzi na CAG mwenyewe, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari. Katika mazungumzo yake, CAG, ambaye alikuwa ameambatana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Serikali Kuu (PAC), Zitto Kabwe na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Serikali za Mitaa (LAAC), Rajab Mbarouk Mohamed, alionyesha jinsi fedha za umma zinavyoendelea kutafunwa, licha ya hati zenye shaka kupungua katika halmashauri nchini.

Wakati wa ukaguzi huo kwa upande wa Serikali za Mitaa, alisema vitabu 2,990 vya stakabadhi za mapato kutoka katika halmashauri 36 havikuonekana na kwamba halmashauri 22, kati ya 134 zilizopo nchini, zililipa Sh bilioni 1.5 ambazo hazikuwa na hati za malipo.

Alisema malipo yenye hati pungufu, yalibainika katika halmashauri 74 ambayo jumla yake ni Sh bilioni 3.3 na kwamba jumla ya Sh milioni 650.3, zililipwa katika halmashauri 20 kwa ajili ya taasisi mbalimbali zilizoko vijijini, ingawa fedha hizo hazikufika zilikokusudiwa.

“Pamoja na hayo, jumla ya Sh milioni 693,132,772, zililipwa kama mishahara kwa wastaafu, watoro, watumishi waliofariki, watumishi walioacha kazi au walioachishwa kazi kupitia akaunti zao na malipo hayo yamehusisha halmashauri 43.

“Kutokana na kuwepo kwa kiwango cha chini cha uzingatiaji wa taratibu na sheria za manunuzi, kulisababisha manunuzi yenye thamani ya Sh milioni 443,107,149 kufanyika katika halmashauri 25 na pia bidhaa zenye thamani ya Sh milioni 541,013,405 ulifanyika bila kibali cha bodi ya zabuni katika halmashauri 24,” alisema CAG.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More