Jumatatu, 29 Aprili 2013

Majaji wamnusuru Jerry Muro na wenzake


MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imemnusuru aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC1), Jerry Murro na wenzake wawili katika hatari ya kesi yao kusikilizwa umpya, badala yake itaendelea kusikilizwa kama rufaa.
Awali kesi hiyo ilikuwa kwenye hatari ya kusikilizwa upya baada ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, kudaiwa kufanya makosa katika utoaji wa hukumu ya Muro na wenzake wawili, Edmund Kapama maarufu kama ‘Dokta’ na Deogratius  Mugassa.
Hata hivyo leo Majaji wa Makahama ya rufaa wametupilia hoja za mawakili wa Serikali waliotoa hoja za kutaka kesi hiyo isikilizwe upya.
Hoja za Jamhuri wakati wa usikilizwaji wa rufaa hiyo, Oktoba 18, mwaka huu, Mawakili wa Serikali, Oswald Tibabyekomya na Awamu Mbangwa, waliiomba mahakama hiyo iamuru kesi hiyo isikilizwe upya chini ya kifungu cha 388 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA).
Wakili Mbangwa alidai kuwa Hakimu aliyesikiliza kesi hiyo (Gabriel Mirumbe) alikosea kisheria katika kuweka kumbukumbu za
mwenendo wa kesi.
Alidai kuwa kutokana na dosari hizo, hata hakimu aliyeandika hukumu ya kesi hiyo (Frank Moshi) aliegemea katika mwenendo huo ambao haukurekodiwa vizuri na matokeo yake alitoa hukumu isiyo sahihi.
Wakili Mbangwa alifafanua kuwa katika mwenendo wa kesi hiyo kuna sehemu za ushahidi wa baadhi ya mashahidi wa upande wa mashtaka, umerekodiwa kwa namna ambayo hauakisi uhalisia wa kile mashahidi hao walichokiziunguza. Aliongeza kuwa kuna baadhi ya sehemu za ushahidi hazikurekodiwa kabisa ikiwemo uamuzi wa mahakama kukataa kupokea kitabu cha wageni waliokuwa wakifika katika hoteli ya Sea Clif ambako Muro na wenzake walidaiwa kukutana na Wage.
Jerry Muro akiwa chini ya Ulinzi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,mwaka 2010Alidai kuwa kutokuwepo kwa uamuzi wa suala hilo katika kumbukumbu kuliinyima nafasi jamhuri kujua sababu za kukataliwa kwa kielelezo hico. Pia alitoa mfano wa maelezo ya onyo ya mjibu rufaa wa kwanza, Muro, kutokuoneshwa kwenye kumbukumbu kuwa yaliopokewa mahakamani hapo. Majibu ya utetezi Wakijibu hoja hizo, mawakili wa utetezi, Richard Rweyongeza na Majura Magafu walidai kuwa malalamiko ya Jamhuri katika hukumu hiyo hayako wazi na kwamba hata kama yapo lakini hawajaonesha jinsi yalivyoathiri hukumu hiyo.
Wakili Magafu alidai kuwa mazingira ya kesi walizozitumia Jamhuri ni tofauti na mazingira ya rufaa hiyo na kwamba kitendo cha Jamhuri kuomba kesi hiyo isikilizwe upya ni sawa na biashara ya kuchagua mahakimu kwamba wakishindwa kwa hakimu mmoja wanakwenda kubahatisha kwa hakimu mwingine. Hata hivyo Wakili wa Serikari Tibabyekomya alidai kuwa hukumu hutokana na ushahidi wa pande zote na kwamba kutokurekodiwa vizuri kwa mwenendo huo na kasoro hizo zilisababisha haki isitendeke kwa pande zote.
Jaji Twaib Jaji Dk Twaib alihoji Jamhuri kama kama mwenendo huo uliochapwa ndivyo ulivyo kwenye mwenendo halisi. Ili kujiridhisha, aliamua kusoma mwenendo halisi uliondikwa kwa mkono, lakini yeye binafsi na hata wakili wa utetezi, Magufu, waalishindwa kuelewa baadhi ya maneno yaliyoandikwa. Baada ya kusikiliza hoja za pande zote Jaji Dk Twaib aliahirisha rufaa hiyo hadi leo kwa ajili ya uamuzi. Muro na wenzake walipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Februari 5, mwaka 2010, na kusomewa mashtaka kula njama na kuomba rushwa kutoka kwa aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Michael Wage.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More