Alhamisi, 2 Mei 2013

TUCTA WATAKIWA KUWABAINISHA WAAJIRI WASIOFUATA SHERIA ZA KAZI

Mkuu wa mkoa wa Arusha magessa Mulongo ameviwataka vyama vya wafanyakazi kuwachunguza waajiri wanao kiuka sheria za kazi kwa kuajiri kwa miezi mitatu mitatu kwani wamekuwa wakiwaacha wafanyakazi kama walivyowaajiri mwanzo bila ya mafao ya mwisho wa kazi tuwakatae waajiri wasiofuta sheria za kazi natoa agizo kuanza kufanya uchunguzi kwa waajiri kama hawa.

Kauli hiyo ameitoa kwenye kilele cha siku ya wafanyakazi kwenye viwanja vya kumbu kumbu ya Sheikh Amri Abeid jijini hapa na kusema kuwa wapo waajiri wa aina hiyo wengi wasiojali maslahi ya wafanyakazi na mwisho wa siku kuwaacha hawana mafao yeyote huko ni kuwaumiza wafanyakazi.

Mulongo alisema kuwa kumekuwapo na wahitimu ambao wenye stashahada na Diploma wamekuwa wakiongoza kwa utendaji mzuri wa kazi wakati wenye digrii wakiwa hawana uzoefu na moyo wakuifanyakazi na kubaki kupiga fitna na wakati wakiwa vyuoni walikuwa wakifuatilia siasa na kuacha kufuta taaluma zilizowapeleka vyuoni humo.

“Ndugu zangu wafanyakazi wenzangu Taaluma yeyote inahitaji muda mzuri wa kuifuatilia tangu ukiwa chuoni hadi unaingia kazini sasa hapa upo chuoni unaacha taaluma unafuata mambo yasio ya taaluma huku ni kutokuwa na wataalamu wa kufaa hapo ndipo fitna zinapoanzia”alisema Mulongo.

Mulongo alienda mbali na kuwataka wanahabari kuandika habari kufuatana na taaluma zao na kuacha ushabiki wa kisiasa kwani taaluma ya uandishi wa habari ni taaluma yenye weledi na ina miiko na maadili hapa ndugu zangu tuelimishe jamii masuala ya kimaendeleo badala ya kijikita kwenye masuala ya kisiasa zaidi na kuicha nchi ikielekea kwenye lingi la vurugu.

“ipo wakati mtajikuta mkiangukia kwenye vyombo vya kisheria kujibu tuhuma mbali mbali kwani mtakuwa mmeacha taaluma na kuuvaa ushabiki wa kisiasa hapo mtakuwa hamuitakii nchini yenu maendeleo bali mtakuwa mnaitakia nchi yenu mabaya”alisema mkuu wa mkoa.

Sherehe hizo zilienda sambamba na maandamano ya vyama vya wafanyakazi na makampuni mbali mbali huku maonyesho ya magari yakitia for a hasa kampuni ya Megatrade Investment watengenezaji wa Kiroba orgin na Kvant Gin na Kiwanda cha Banana Ivestment Huku kwenye viwanda vya kutengeneza nguo Kampuni ya AtoZ ikitia for a ikifuatiwa na kampuni ya Sunflag zote za jijini hapa.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More