
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi
(kushoto), akiwa bungeni mjini Dodoma. Kulia ni Mbunge wa Sengerema,William Ngeleja.
HABARI zilizotoka bungeni mjini Dodoma muda huu ni kwamba matokeo
yote ya kidato cha nne 2012 yamefutwa na mitihani itasahihishwa upya
haraka iwezekanavyo.
Taarifa ya tume iliyoundwa na Waziri Mkuu,
Mizengo Pinda kuchunguza sababu za kufeli vibaya kwa watahiniwa wa
kidato cha nne kwa mwaka jana imesomwa leo bungeni na Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi.
Waziri Lukuvi amesema sababu zilizosababisha wanafunzi hao kufeli ni
pamoja na upungufu wa waalimu, mazingira magumu ya kufundishia, idadi
kubwa ya shule za sekondari iliyopelekea idadi kubwa ya watahiniwa na
utaratibu mbovu wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) uliotumika
bila kuwashirikisha wadau mbalimbali wa elimu.
Kutokana na sababu hizo, matokeo yote ya kidato cha nne 2012 yamefutwa na mitihani itasahihishwa upya.
Posted in:
0 maoni:
Chapisha Maoni